Tuesday, October 15, 2024

RAIS WA UTPC AKIJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA


Rais wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) Deogratius Nsokolo, amejiandikisha katika daftari la wakazi katika kitongoji cha Kabatini kijiji cha Isinde katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba 27 mwaka huu.


Nsokolo ametoa wito kwa waandishi wa habari nchini kuendelea kuhamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha ili waweze kuchagua viongozi wanaowataka watakaosaidia kuleta maendeleo katika maeneo yao.

No comments:

Post a Comment