Friday, March 29, 2024

POLISI KATA AWAREJESHA SHULE IRENE NA AGIZO

 

Polisi Kata ya Kinyala iliyopo Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Lusajo Kibonde Machi 28, 2024 alifanikiwa kuwarejesha shuleni kuendelea na masomo wanafunzi wawili wa darasa la saba Irene Mwakwilusa na Agizo Anyimike.

Awali wanafunzi hao walikuwa wakisoma katika Shule ya Msingi Ikukisya iliyopo Wilaya ya Rungwe lakini kutokana na changamoto mbalimbali na hali duni ya maisha waliacha Shule.

Machi 01, 2024 Polisi Kata ya Kinyala Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Lusajo Kibonde baada ya kupata taarifa za uwepo wa watoto hao, alilazimika kuitembelea familia hiyo na kufanya mazungumzo na mama mzazi wa watoto hao Bi. Christina Mwamengo.

Jitihada mbalimbali zilifanyika ikiwa ni pamoja na kununua mahitaji ya Shule ya watoto hao na Machi 28, 2024 wamerejea shuleni na kuungana na wanafunzi wenzao kuendelea na masomo katika Shule ya Msingi Igembe iliyopo Wilaya ya Rungwe.


No comments:

Post a Comment