Tuesday, October 1, 2024

DKT. TULIA ACHANGIA MIFUKO 100 YA SARUJI KWAAJILI YA UJENZI WA OFISI YA SERIKALI YA MTAA

Spika wa Bunge na Mbunge Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson amechangia mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya serikali ya Mtaa Kata ya Isanga Jijini hapa.

Mbali na kuchangia ujenzi huo pia amefanya ziara ya kukagua ujenzi wa zahanati ya kata hiyo sambamba na  kufungua ofisi ya bodaboda  eneo la Ilemi Jijini hapa.

Akizungumza na mamia ya wananchi leo Oktoba mosi Dkt. Tulia amesema kuwa serikali itaendelea kuboresha miradi ya maendeleo kama kutekeleza ilani ya uchaguzi 2024/25.

Amesema pia serikali imewekeza zaidi ya Sh 11 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Mama na Mtoto katika Hosptali ya Rufaa Kanda kitengo cha Wazazi Meta.

Naye Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya na Diwani wa kata ya Isanga Dour mohamed Issa amesema  kwa kipindi cha uongozi wa  Dkt. Tulia wamepata miradi mbalimbali kama miundombinu ya barabara, zahanati.

"Tuna kila sababu ya kujivunia uwepo wa Mbunge Dkt. Tulia tumepokea miradi mbalimbali ambayo imekuwa mwarobaini na tija kubwa kwa  wananchi".


Mkazi wa Isanga Stella Joel ameomba serikali kuharakishwa ujenzi wa zahanati ya kata ili kuokoa wakinamama wajawazito kutembea umbali mrefu kufuata huduma.

No comments:

Post a Comment