Tuesday, October 1, 2024

BODOBODA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA BARABARANI

Mbunge Jimbo la Mbeya Mjini ambaye ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Dkt. Tulia Ackson amezindua Jengo la Ofisi ya Bodaboda Kanda ya Soweto Mbeya Mjini huku akisisitiza kutii sheria za usalama barabarani.

Ofisi hiyo imejengwa katika Mtaa wa James Kata ya Ilemi kwa Jitihada za Wanachama wa Bodaboda Kanda ya Soweto ili iwasaidie katika Shughuli mbalimbali za Kiofisi na kuwaongezea kipato kupitia Vyumba vya Biashara vilivyojengwa kwenye Ofisi hiyo.

Dkt. Tulia amewaasa Madereva Bodaboda kufuata Sheria za Usalama Barabarani na kutumia vizuri vyombo vyao vya Moto katika kujitafutia kipato na sio uhalifu ili kutimiza Malengo yao kama ambavyo wamefanikisha kujenga Ofisi hiyo.

Aidha Dkt. Tulia amewataka Wananchi  wajitokeza kujiandisha kwenye Daftari la Mpiga Kura ili waweze kutimiza haki yao ya kupiga kura kuwachagua Viongozi wa Serikali za Mitaa katika Uchaguzi Utakaofanyika Mwezi Oktoba Mwaka huu.


No comments:

Post a Comment