Njiku ametoa rai hiyo wakati akizungumza na waandishi wa
habari kuhusu maandalizi ya chama hicho kuelekea uchaguzi wa
Serikali za mitaa, vitongoji na vijiji utakaofanyika Novemba 27, 2024.
"Tumeona muamko mdogo wa watu kujitokeza kupiga kura lakini niwambie hii ni haki yetu ili kupata viongozi bora kwa maendeleo ya taifa letu", amesema Ipyana Njiku.
Pia Njiku amewataka wananchi kuwa chachu ya kutunza amani
ya nchi wakati na baada ya chaguzi ili kuendelea kuwa Taifa moja na
kuwaalika wenye nia na uwezo kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali kupitia chama hicho.
"Haki ya kupiga kura ni silaha muhimu kwa kila raia katika kuhakikisha uongozi bora maendeleo yetu, bila kura unatoa nafasi kwa wengine kuamua nani awe kiongozi wao kwahiyo tunaomba siku ya uchaguzi tujitokeze kwa wingi kwenda kuchagua viongozi bora. Pamoja na kupiga kura lakini hii ni fursa kwa watu wenye sifa, dhamira safi, uadilifu na utayari kuwatumikia wananchi kwa kujitokeza kugombea kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma CHAUMMA", amesema Njiku.
No comments:
Post a Comment