Tuesday, October 1, 2024

MBUNGE MASACHE AZINDUA MASHINDANO AMBWENE CUP

Mbunge wa Jimbo la Lupa Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya Masache Kasaka amezindua mashindano ya Ambene Cup 2024 yanayotimua kivumbi katika viwanja vya Matundasi "A".

Mashindano hayo yatashirikisha timu 32 huku yakifunguliwa na timu ya Chokaa FC na kisimani FC zote za wilayani Chunya katika kipindi cha kwanza cha mchezo.

Imeelezwa timu zitakazo ibuka kidedea zitajinyakulia kitita cha fedha huku  mbalimba mshindi wa kwanza  Sh 5 milioni wa pili Sh 3 milioni wa tatu Sh 2 milioni huku wa nne shilingi milioni moja.

Akizungumza mara baada ya kuzindua mashindano hayo Masache ametaka ukawe wa haki bila kupendelea upande wowote na vijana kutumia kama fursa ya ajira na kiuchumi.


No comments:

Post a Comment