Sunday, October 12, 2025

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA UYOLE AFANYA KAMPENI MGUU KWA MGUU

 

Mgombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Ipyana Samson Njiku, ameendelea na kampeni zake za mguu kwa mguu kwa wananchi wa Jimbo la Uyole, ambapo leo ametembelea maeneo ya Kata ya Itezi na Igawilo akiwahamasisha wananchi kujiandaa kwa mabadiliko chanya kupitia uongozi makini na wenye dira ya maendeleo.

Akizungumza na wananchi katika maeneo mbalimbali , Njiku amesema kuwa endapo atapata ridhaa ya wananchi wa Uyole, ataweka kipaumbele katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo:

Ujenzi wa Soko la Kisasa na Kimataifa litakalowezesha wakulima na wafanyabiashara kuuza mazao yao ndani na nje ya nchi kwa urahisi, kuongeza ajira na kipato cha wananchi.

Monday, August 25, 2025

PATRIC MWALUNENGE ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINI

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ameteuliwa na chama hicho kugombea nafasi ya ubunge wa jimbo la Mbeya Mjini, leo Agosti 25, 2025 amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.

MWANDISHI WA HABARI KUCHUANA NA SPIKA TULIA, UBUNGE JIMBO LA UYOLE



Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma Taifa, Ipyana Samson Njiku, leo Agosti 25, 2025 amechukua fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia chama hicho.

Ipyana amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira yake ya kuwatumikia wananchi wa Uyole kwa uadilifu, uwajibikaji na kusimamia maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Amesisitiza kuwa chama chake kimejipanga kutoa mbadala mpya wa kiuongozi unaolenga kuleta matumaini mapya kwa wananchi.


Tuesday, July 29, 2025

Saturday, July 26, 2025

MWAKIPESILE AMPONGEZA DKT. SAMIA KWA KUENDESHA MKUTANO KIDIGITALI

AJALI YAUA WANAFUNZI WATANO WAKIKIMBIA MCHAKAMCHAKA, CHUNYA MBEYA


Wanafunzi watano wa Sekondari ya Chalangwa Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya wamefariki kwa kugongwa na basi lenye namba za usajili namba T 194 DCE aina ya YUTONG linalomilikwa na Kampuni ya Safina linalofanya safari zake Lualaje Mbeya Julai 26, 2025 majira ya saa 11:30 alfajiri barabara kuu ya Chunya Mbeya.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ACP Wilbert Siwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo wanafunzi watano wamefariki papo hapo na majeruhi tisa wamepokelewa Kituo cha Afya Chalangwa.

Siwa amesema mara baada ya tukio dereva wa basi hilo alitoroka na juhudi za kumtafuta zinaendelea ambapo ametoa wito kwa madereva kuwa waangalifu wawapo barabarani na chanzo kikitajwa ni mwendo kasi na uzembe wa dereva.

Thursday, July 17, 2025

TULIA TRUST YAREJESHA TABASAMU FAMILIA NYUMBA ILIYOTEKETEA MOTO


Taasisi ya Tulia Trust inayojihusisha na uwekezaji  kiuchumi wananchi imeanza ukarabati wa nyumba ya familia ya Mzee Ayoub Wakazi wa Kata ya Nsalaga Jijijini hapa.

Nyumba hiyo iliteketea kutokana na janga la moto lililotokea hivi karibuni hali iliyosababisha kukosa mahala pa kuishi.


Ukarabati huo unatekelezwa na Taasisi ya Tulia Trust  ambayo Mkurugenzi wake ni Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson na Rais wa Mabunge Duniani (IPU), kupitia mpango wa Tulia Trust mtaani kwetu.

Mpango huo umekuwa na tija ya kurejesha tabasamu kwa wananachi wa Jiji la Mbeya zikiwepo kaya zisizojiweza, yatima na wazee.

Thursday, July 10, 2025

MAHAKAMA YATUPILIA MBALI KESI YA MDUDE

Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya imetupilia mbali maombi ya jinai namba 14538/2025 yaliyofunguliwa mei 17,2025 na Sije Mbughi mke wa Mpaluka Nyagali (Mdude) dhidi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Mkurugenzi wa mashitaka (DPP), Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya(RPC), Mkuu wa upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO) na askari Shaban Charo anayedaiwa kuwa ndiye aliyemchukua Mdude ambapo maombi yameanza kusikilizwa Juni 30, 2025 na kutolewa uamuzi Julai 9, 2025 na Jaji Said Kalunde.

Mleta maombi Sije Mbughi amewakilishwa na Wakili Bonifase Mwabukusi, Wakili Hekima Mwasipu na Wakili Solomon Kamunyu ambapo upande wa wajibu maombi umewakilishwa na Wakili Domick Mushi pamoja na Wakili Adalbert Zegge huku Sije akitaka mumewe kufikishwa mahakamani na kufungulia mashitaka kwa mujibu wa sheria.

Jaji Said Kalunde ameanza kutoa uamuzi majira ya saa 9:35 alasiri na kuhitimishwa saa 11:50 jioni awali Jaji Said Kalunde amesema upande wa mleta maombi akiwemo Sije Mbughi na Ezekiel Sheyo.

Monday, June 30, 2025

MASACHE ACHUKUA FOMU YA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE WA JIMBO LA LUPA, CHUNYA

Mbunge wa Jimbo la Lupa Masache Kasaka amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea nafasi ya ubunge wa Jimbo hilo kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM leo Juni 30, 2025.


 

MWALUNENGE AREJESHA FOMU YA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINI

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mbeya Patrick Mwalunenge amerejesha fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kugombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Mbeya Mjini leo Juni 30, 2025.



 

Sunday, June 29, 2025

MHANDISI MARYPRISCA MAHUNDI ACHUKUA FOMU KUTETEA NAFASI YAKE

Mhandisi Maryprisca Mahundi amefika katika ofisi za UWT Mkoa wa Mbeya kuchukua fomu ya kugombea Ubunge Viti Maalum Mkoa wa Mbeya.

Mhandisi Maryprisca Mahundi amechukua fomu hiyo ili kutetea nafasi yake ambayo ameitumikia muhula mmoja wa miaka mitano (2020-2025).

 

MWANAHABARI AJITOSA KUMKABILI MEYA WA JIJI LA MBEYA

Mwandishi wa Habari, David Nyembe (kushoto), akikabidhiwa fomu ya kuomba ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Isanga kuchaguliwa kuwa mgombea udiwani wa Kata hiyo katika Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba mwaka huu.

Nyembe amekabidhiwa fomu na Katibu wa CCM Kata hiyo Golden Ndolela leo Juni 29, 2025.


Hadi kufikia leo majira ya saa nne asubuhi jumla ya wagombea watatu tayari wamechukua fomu ya kuomba ridhaa ya chama hicho kuwania nafasi hiyo akiwemo aliyekuwa Meya wa Jiji la Mbeya Mh. Dormohamed Issa.