Monday, June 29, 2026

RIPOTI MAALUM: KUTOKA MOTO WA KUFUKUZA FISI HADI MWANGA WA UMEME

 Umeme wageuza vijiji kuwa vituo vya maendeleo; shule, biashara na kilimo vyanufaika…

Na Sanula Athanas aliyekuwa Shinyanga

 


Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Masunula, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, wakisoma TEHAMA kwa vitendo katika moja ya madarasa ya shule hiyo hivi karibuni. Sekta ya elimu imenufaika na ujio wa umeme vijijini. PICHA: SANULA ATHANAS

KIJIJI cha Masunula katika Kata ya Usule, Wilaya ya Shinyanga mkoani Shinyanga, kina historia inayofanana na mamia ya vijiji vingine nchini.

Kilianzishwa mwaka 1974 kupitia Operesheni Vijiji (1973-1976), mkakati wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, uliolenga kuwakusanya wananchi katika maeneo maalum ili kurahisisha utoaji huduma za msingi kama elimu, afya, maji na miundombinu mingine ya maendeleo.

Kwa miongo mitano, wakazi wa Masunula waliishi maisha ya kawaida ya vijijini yaliyotawaliwa na matumizi ya mafuta ya taa kwa mwanga, mashine zinazotumia dizeli kwa shughuli za uzalishaji na uhaba wa huduma nyingi za kisasa zilizokuwa zikionekana kama haki ya wakazi wa mijini pekee.

RIPOTI MAALUM: JINSI TANZANIA INAVYOJINASUA KUTOKA UTEGEMEZI WA MAFUTA

Vituo 50 vya kuchaji magari ya umeme kusimikwa katika mikoa yote nchini, serikali yapanga kununua magari ya umeme na kuhamasisha matumizi ya gesi asilia

 

Na Sanula Athanas aliyekuwa Dodoma 

Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, akiwa pamoja na viongozi wengine, akiweka jiwe la msingi wakati wa uzinduzi wa kituo cha kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme katika Ofisi za Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) jijini Dodoma, Juni 11 mwaka huu. PICHA: SANULA ATHANAS

 

KILA siku, Juma Mwinuka (29) huamka alfajiri na kuanza kazi yake ya kubeba abiria kwa bajaj katika eneo la Kimara Golani, jijini Dar es Salaam.

Kwa miaka mingi alikuwa akitumia bajaj inayotumia petroli, jambo lililomlazimu kutumia kati ya Sh. 20,000 na 25,000 kwa siku kununua mafuta.

Lakini leo maisha yake yamebadilika. Akiwa ameketi katika bajaj yake ya umeme, Mwinuka anasema ameshuhudia tofauti kubwa kati ya teknolojia ya zamani na mpya. 

“Nilikuwa natumia Sh. 20,000 hadi 25,000 kwa siku kununua petroli. Sasa nachaji bajaj yangu kwa gharama isiyozidi Sh. 8,000 kwa siku,” anasema huku akitabasamu.

Sunday, October 12, 2025

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA UYOLE AFANYA KAMPENI MGUU KWA MGUU

 

Mgombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Ipyana Samson Njiku, ameendelea na kampeni zake za mguu kwa mguu kwa wananchi wa Jimbo la Uyole, ambapo leo ametembelea maeneo ya Kata ya Itezi na Igawilo akiwahamasisha wananchi kujiandaa kwa mabadiliko chanya kupitia uongozi makini na wenye dira ya maendeleo.

Akizungumza na wananchi katika maeneo mbalimbali , Njiku amesema kuwa endapo atapata ridhaa ya wananchi wa Uyole, ataweka kipaumbele katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo:

Ujenzi wa Soko la Kisasa na Kimataifa litakalowezesha wakulima na wafanyabiashara kuuza mazao yao ndani na nje ya nchi kwa urahisi, kuongeza ajira na kipato cha wananchi.

Monday, August 25, 2025

PATRIC MWALUNENGE ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINI

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ameteuliwa na chama hicho kugombea nafasi ya ubunge wa jimbo la Mbeya Mjini, leo Agosti 25, 2025 amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.

MWANDISHI WA HABARI KUCHUANA NA SPIKA TULIA, UBUNGE JIMBO LA UYOLE



Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma Taifa, Ipyana Samson Njiku, leo Agosti 25, 2025 amechukua fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia chama hicho.

Ipyana amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira yake ya kuwatumikia wananchi wa Uyole kwa uadilifu, uwajibikaji na kusimamia maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Amesisitiza kuwa chama chake kimejipanga kutoa mbadala mpya wa kiuongozi unaolenga kuleta matumaini mapya kwa wananchi.


Tuesday, July 29, 2025

Saturday, July 26, 2025

MWAKIPESILE AMPONGEZA DKT. SAMIA KWA KUENDESHA MKUTANO KIDIGITALI

AJALI YAUA WANAFUNZI WATANO WAKIKIMBIA MCHAKAMCHAKA, CHUNYA MBEYA


Wanafunzi watano wa Sekondari ya Chalangwa Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya wamefariki kwa kugongwa na basi lenye namba za usajili namba T 194 DCE aina ya YUTONG linalomilikwa na Kampuni ya Safina linalofanya safari zake Lualaje Mbeya Julai 26, 2025 majira ya saa 11:30 alfajiri barabara kuu ya Chunya Mbeya.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ACP Wilbert Siwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo wanafunzi watano wamefariki papo hapo na majeruhi tisa wamepokelewa Kituo cha Afya Chalangwa.

Siwa amesema mara baada ya tukio dereva wa basi hilo alitoroka na juhudi za kumtafuta zinaendelea ambapo ametoa wito kwa madereva kuwa waangalifu wawapo barabarani na chanzo kikitajwa ni mwendo kasi na uzembe wa dereva.

Thursday, July 17, 2025

TULIA TRUST YAREJESHA TABASAMU FAMILIA NYUMBA ILIYOTEKETEA MOTO


Taasisi ya Tulia Trust inayojihusisha na uwekezaji  kiuchumi wananchi imeanza ukarabati wa nyumba ya familia ya Mzee Ayoub Wakazi wa Kata ya Nsalaga Jijijini hapa.

Nyumba hiyo iliteketea kutokana na janga la moto lililotokea hivi karibuni hali iliyosababisha kukosa mahala pa kuishi.


Ukarabati huo unatekelezwa na Taasisi ya Tulia Trust  ambayo Mkurugenzi wake ni Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson na Rais wa Mabunge Duniani (IPU), kupitia mpango wa Tulia Trust mtaani kwetu.

Mpango huo umekuwa na tija ya kurejesha tabasamu kwa wananachi wa Jiji la Mbeya zikiwepo kaya zisizojiweza, yatima na wazee.

Thursday, July 10, 2025

MAHAKAMA YATUPILIA MBALI KESI YA MDUDE

Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya imetupilia mbali maombi ya jinai namba 14538/2025 yaliyofunguliwa mei 17,2025 na Sije Mbughi mke wa Mpaluka Nyagali (Mdude) dhidi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Mkurugenzi wa mashitaka (DPP), Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya(RPC), Mkuu wa upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO) na askari Shaban Charo anayedaiwa kuwa ndiye aliyemchukua Mdude ambapo maombi yameanza kusikilizwa Juni 30, 2025 na kutolewa uamuzi Julai 9, 2025 na Jaji Said Kalunde.

Mleta maombi Sije Mbughi amewakilishwa na Wakili Bonifase Mwabukusi, Wakili Hekima Mwasipu na Wakili Solomon Kamunyu ambapo upande wa wajibu maombi umewakilishwa na Wakili Domick Mushi pamoja na Wakili Adalbert Zegge huku Sije akitaka mumewe kufikishwa mahakamani na kufungulia mashitaka kwa mujibu wa sheria.

Jaji Said Kalunde ameanza kutoa uamuzi majira ya saa 9:35 alasiri na kuhitimishwa saa 11:50 jioni awali Jaji Said Kalunde amesema upande wa mleta maombi akiwemo Sije Mbughi na Ezekiel Sheyo.

Monday, June 30, 2025

MASACHE ACHUKUA FOMU YA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE WA JIMBO LA LUPA, CHUNYA

Mbunge wa Jimbo la Lupa Masache Kasaka amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea nafasi ya ubunge wa Jimbo hilo kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM leo Juni 30, 2025.


 

MWALUNENGE AREJESHA FOMU YA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINI

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mbeya Patrick Mwalunenge amerejesha fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kugombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Mbeya Mjini leo Juni 30, 2025.