Thursday, October 3, 2024

MEYA ISSA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA TACTIC

Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya Dourmohamed Issa leo amefanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya Soko la Kisasa la Matola  na mitaro ya kutililisha Maji ya Mvua  katika Kata ya Nzovwe.

Miradi hiyo inatekelezwa kupitia Mradi wa kuboresha majiji (TACTIC) ambayo iko katika hatua nzuri za utekelezaji.


Akizungumza na Mwandishi wa habari leo mara baada ya kufanya ziara hiyo, Issa ameipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Sami Suluhu Hassan kwa kuleta miradi mikubwa ya kimkakati Jijini hapa.

"Kipindi cha miaka mitatu ya Rais Samia Suluhu Hassan na Mbunge wa Mbeya mjini, Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson wanaona Mkoa wa Mbeya unakwenda kasi katika miradi ya maendeleo" amesema Issa.


Amesema amekuwa Meya wa IPU kwani miradi inatekelezwa kwa kasi ukiachia ujenzi wa soko na mifereji pia kuna ujenzi wa kituo kikubwa cha kisasa cha mabasi ya mikoani ambacho kitakuwa chachu ya fursa za kiuchumi na mwingiliano wa shughuli za kiuchumi.

No comments:

Post a Comment