Thursday, July 4, 2024

TAASISI YA TULIA TRUST IMETOA BANDO TISA ZA BATI UJENZI WA UKUMBI

Taasisis ya Tulia Trust umekabidhi msaada wa mabati bando tisa za bati kwa ajili ya ujenzi wa ukumbi wa  ofisi ya chama cha Mapinduzi shina namba nane kata ya Iyela Jijini hapa.

Msaada huo wa Mabati umetolewa na Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Mbeya mjini Spika wa Bunge na Rais wa Umoja wa Mabunge (IPU) Dkt. Tulia Ackso Ackson, Steven Chambanenge.

Amesema kuwa Dkt. Tulia amekuwa na mapenzi mema kwa wanambeya na kuwataka asifanye makosa unapofika wakati kwa kupiga kura za kishindo kwa Rais Samia Suluhu Hassan na Mbunge wao Dkt. Tulia Ackson.


Kwa upande wake Mjumbe wa shina namba nane, Gaporic Lwibha amesema anamshukuru Mbunge wa Jimbo la Mbeya mjini na Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson kwa kuchangia ujenzi wa ukumbi huo.

"Ndugu zangu tulitumia muda mfupi sana kuomba lakini leo hii tumekabidhiwa, naomba Katibu wa Mbunge nifikishie salama za shukrani zetu kuna majibu yake 2025 kwake Rais Samia Suluhu Hassan" amesema.

No comments:

Post a Comment