Friday, July 12, 2024

DKT. TULIA NA RAIS WA URUSI WAJADILI NAMNA BORA YA KUIMARISHA AMANI DUNIANI

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson,  amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Urusi, Vladimir Putin Jijini St. Petersburg nchini Urusi leo Julai 12, 2024 ambapo katika mazungumzo yao wamejadili kuhusu namna bora ya kuimarisha amani Duniani.

“Kabla ya kuzungumza naye tayari tulishazungumza na Maspika wa nchi zote hizo mbili na sisi kama Umoja wa Mabunge Duniani tumezungumza naye kama Kiongozi wa nchi katika sura ambayo tunaweza kuziweka pamoja nchi zote mbili na tutarajie kwamba IPU itatengeneza fursa ya Mabunge ya pande zote ili kuweza kuzungumzia amani katika maeneo yao ya utawala” amesema Dkt. Tulia.


No comments:

Post a Comment