Friday, March 8, 2024

UMOJA WA WANAWAKE MZRH WAKABIDHI HUNDI YA MIL. 37.5 KWAAJILI YA UNUNUZI WA KITANDA CHA KISASA CHA UPASUAJI WA MIFUPA

Ikiwa ni kiliele cha Madhimisho ya Siku ya Wanamke Duniani ambayo huadhimishwa machi 8 kila mwaka, Umoja wa Wanawake Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya leo Machi 08, 2024 wamekabidhi hundi yenye thamani ya shilingi Mil 37.5 kwaajili ya ununuzi wa kitanda cha kisasa kwaajili ya Upasuaji wa mifupa hospitalini hapo.

Akipokea hundi hiyo ya Mil 37.5 Dkt. Godlove Mbwanji ,Mkurugenzi Mtendaji wa Hospotali ya Rufaa ya Kanda Mbeya ameushukuru na kuupongeza Umoja wa Wanawake Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kwa kuwa chachu na mchango mkubwa katika maendeleo ya Hospitali na mkoa kwa ujumla.

“...ninyi mmekuwa ni chachu kubwa sana kwa mafanikio ya hospitali na mkoa kwa ujumla nichukue nafasi hii pia kuwapongeza wanawake wote Tanzania nzima kwa mchango mkubwa sana wa maenedeleo ya nchi yetu.” Dkt. Godlove mbwanji

Sambamba na hilo Dkt. Mbwaji ametoa rai kwa akina baba kuweka jitahada zaidi katika malezi ya mtoto wa kiume ili kujenga taifa lenye vijana imara katika jamii.

“...lakini sasa hebu tuwatazame watoto wa kiume na hii sio kwa akina mama ni kwa upande wa akina baba pia ili mwisho wa siku tuwe na taifa lenye vijana imara.” Dkt. Godlove Mbwanji.
 
Akiongea wakati wa kukabidhi hundi hiyo, Joyce Komba, katibu wa umoja huo amesema lengo la kukabidhi zawadi hiyo ni kurudisha fadhila kwa jamii pamoja na kuushukuru Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kwa kuwaongoza katika misingi imara inayopelekea kutoa huduma bora kwa wagonjwa na kudumisha umoja, upendo na mshikamo.
 “..zawadi hii ni sehemu ya kurudisha fadhila kwa jamii pamoja na kushukuru uongozi wa hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kwa kutujenga katika misingi imara pamoja na kudumisha umoja na mshikamano kwa watumishi” Joyce Komba

Dkt. John Mbanga ni mkuu wa idara ya upasuaji hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, ameshukuru kwa zawadi hiyo na kusema upatikanaji wa kitanda hicho umekuwa msaada mkubwa sana hasa katika kipindi ambacho ajali zimekuwa nyingi na kusema kitanda hicho ni cha kipekee na kisasa kitakachopelekea huduma ya upasuaji wa mifupa kufanyika kwa urahisi zaidi.

No comments:

Post a Comment