Madereva
wa Magari ya mizigo, abiria na viongozi wametakiwa kuzingatia na kufuata sheria, alama, ishara na michoro ya
usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.
Kauli
hiyo imetolewa leo Machi 25, 2024 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga wakati
akifungua mafunzo ya muda mfupi kwa madereva wa magari ya mizigo, abiria
na viongozi katika Chuo cha udereva cha Agility Professional Driving
School (APDS) cha Jijini Mbeya.
Pia,
Kamanda Kuzaga amewataka madereva wanafunzi kuheshimu watumiaji wengine
wa barabara kwani nao wana haki ya kutumia barabara.
"Mbali
ya vyombo vya moto kuna watumiaji wengine wa barabara, walemavu,
watoto, wenye uoni hafifu na viziwi, hao nao wana haki ya kutumia
barabara, waheshimuni kwa kuhakikisha mnafuata sheria, alama, ishara na
michoro iliyopo barabarani " alisema Kuzaga.
Mkufunzi
Mhandisi David Mtunguja kutoka chuo cha ufundi Arusha amesisitiza suala
la umuhimu wa Dereva kulijua gari lake ili kuepuka ajali ambazo zaidi
ya asilimia 70 zinasababishwa na uzembe wa madereva.
Mkurugenzi wa Agility Professional Driving School Mhandisi Anthony
Malamla ameomba Serikali kuongeza nguvu ya udhibiti wa vyuo vya udereva
ambavyo havijakidhi vigezo wala kusajiliwa ili kuepuka utapeli na
kuzalisha madereva wasio na weledi katika taaluma ya udereva.
Jumla
ya madereva wanafunzi 16 wa magari ya mizigo, abiria na viongozi (VIP
Course) kutoka mikoa ya Mbeya, Mwanza na Arusha wamefungulia rasmi
mafunzo ya udereva ya muda mfupi katika chuo hicho kwa lengo la
kuwajenga uwezo na weledi katika matumizi sahihi ya barabara.
No comments:
Post a Comment