Afisa
 Tarafa ya Ilongo Magdalena Sikwese  ameagiza Maafisa Watendaji wa 
Kata na Vijiji kuhakikisha wanatumia nafasi zao kwa kuwatumikia Wananchi
 vizuri ikiwemo kuwa na kauli nzuri, kuwa wakarimu, kusoma mapato kwa 
wananchi, kusikiliza na kutatua  kero za Wananchi.
"Watendaji 
tumeshau wajibu wetu wa kusoma mapato na matumizi.  Sisi Watendaji 
tumefika kwenye maeneo ya Wananchi tukajifanya nasisi wananchi, 
tumesahau kwamba hao Wananchi tumewafahamu baada ya kupata ajira hapo." 
Sikwese amesema unaposoma taarifa za mapato na matumizi kwa Wananchi inatia 
moyo hata utakapowaomba michango mingine ya kimaendeleo itakuwa rahisi 
kujitoa.
.jpg)
Pia Sikwese amesema kila mtu akitimiza wajibu wake 
ipasavyo, basi Tarafa ya Ilongo itakuwa na maendeleo huku akikemea tabia
 ya baadhi ya Watendaji kuwajibu vibaya Wananchi pale wanapohitaji 
huduma kutoka kwao.
Sikwese amewataka Watendaji kuacha tabia ya kukataa 
kuwasikiliza Wananchi hata kama wamefika muda wa kuchelewa kwakuwa 
Wananchi wanaamini Watendaji ndio  jawabu la mwisho kuhusu shida zao na 
kutegemea msaada zaidi.
Kwa upande mwingine, baada ya Watendaji 
wa Kata na Maafisa Elimu kuwasilisha taarifa zao za utekelezaji wa 
maendeleo katika kata zao,  idadi ya Watendaji wa vijiji waliohudhulia 
kikao hicho haikuwa ya kuridhisha na kupelekea Sikwese kutoa tamko 
la kuwaorodhesha Watendaji wote wa vijiji ambao hawajahudhulia.
Hata 
hivyo, aliwaomba Watendaji wa vijiji kuwasilisha taarifa zao za 
utekelezaji lakini chakushangaza wengi hawakuwa na taarifa za 
utekelezaji. Sikwese  amegiza Watendaji wote wa vijiji ambao 
hawajahudhulia kikao cha leo waandike barua za maelezo na nakala iende 
kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali.
Vilevile
 hakusita kukemea tabia ya Watendaji pamoja na Maafisa wengine kuvaa 
mavazi yasiyo rasmi wawapo maofsini. Amesema iwe marufuku uvaaji wa 
mavazi aina ya Dera au nguo za kubana ( jinsi za kubana), viatu vya wazi
 (open shoes au sandal)  pamoja mabuti (Rain boots), huku akisisitiza 
sana kuacha kufanya kazi kwa mazoea.
.jpg)
.jpg)
.jpg)
No comments:
Post a Comment