Friday, March 22, 2024

MAMLAKA YA MAJI MBEYA KUTUMIA MIKUTANO YA HADHARA KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya imeshiriki mkutano wa kusikiliza kero za wananchi katika he Kata ya Maanga.

Ofisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo Neema Stanton amesema lengo ni kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya maji, usomaji wa dira shirikishi, matumizi sahihi ya majisafi ili kuepuka ankara kubwa ya maji inayotoka na utumiaji wa maji isivyo sahihi.

Ametumia fursa hiyo kuwaomba wananchi kutumia mfumo wa majitaka kwa usahihi kwa kuacha kutupa taka ngumu kwenye mfumo ambazo hupelekea mifumo ya majitaka kuziba na kuhatarisha afya za wananchi.

Pia Mamlaka imewataka wateja kutoa taarifa kwapale wanapokutana na changomoto ikiwepo watu wanaojihusisha kujiunganishia Maji kwa njia za kificho.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji, Mhandisi Barnabas Konga amesema kufuatia elimu inayotolewa ya wateja kuunganisha huduma hiyo mpaka sasa wamepokea maombi zaidi ya 700.

No comments:

Post a Comment