Friday, March 8, 2024

MTANDAO WA POLISI WANAWAKE WAWA KIVUTIO MAADHIMISHO SIKU YA WANAWAKE DUNIANI


Mtandao wa Polisi Wanawake Mkoa wa Mbeya (TPF Net) ukiongozwa na Mwenyekiti wake Mrakibu wa Polisi (SP) Kaneng Muro umepamba kilele cha maadhimisho ya siku ya mwanamke dunia ambayo kimkoa yamefanyika Ubaruku, Wilaya ya Mbarali.

Katika maadhimisho hayo, Mtandao wa Polisi Wanawake umeshiriki katika maandamano yaliyohusisha Taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za Serikali ambayo yalibeba jumbe mbalimbali.

Pia, mtandao wa Polisi wanawake mkoani hapa  kwa kushirikiana na Dawati la Jinsia na Watoto umekuwa kivutio kwa washiriki wa maadhimisho hayo ambapo elimu kuhusu masuala ya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji dhidi ya watoto na wanawake ilitolewa.

Sambamba na hilo, kikosi cha usalama barabarani kilipata nafasi ya kueleza matumizi ya kidigitali ya ukusanyaji wa madeni ya makosa ya usalama barabarani, vipimo vya ulevi kwa madereva na ukamataji wa makosa ya ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani kwa kutumia "POS Machine".

Mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya siku ya mwanamke dunia kwa Mkoa wa Mbeya alikuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Kanali Denis Mwila kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera huku maadhimisho yamebeba kauli mbiu "Wekeza kwa Wanawake, Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii".


No comments:

Post a Comment