Mbalaza wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa
kutoka Mkoa wa Mbeya Timida Fyandomo ametembelea eneo la ujenzi wa
nyumba ya muhitaji anayejengewa na taasisi ya Tulia Trust katika kata ya
Iganjo Mbeya Mjini.
Akiwa katika eneo hilo Timida ameahidi kutoa
Godoro kumsaidia muhitaji huyo ikiwa ni kuunga mkono jitihada
zinazofanywa na Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi wake ambaye
ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Spika wa Bunge na Mbunge wa
Jimbo la Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson.
Nyumba hiyo inayojengwa kupitia mpango wa Tulia Trust Mtaani Kwatu
inatarajiwa kukabidhiwa kwa mlengwa huyo mapema mweezi Aprili mwaka huu.
Kwa
upande wake, Ofisa Habari na Mawasiliano wa Taasisi ya Tulia Trust,
Joshua Mwakanolo amesema ujenzi wa nyumba hiyo iko katika hatua za
mwishoni.
Amesema wanatarajia mara baada ya kukamilisha ujenzi
huo uzinduzi utafanywa na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Spika
wa Bunge na Mbunge Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson ambaye pia ni
Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust.
No comments:
Post a Comment