Thursday, March 28, 2024

TIMIDA FYANDOMO KUMCHANGIA GODORO MJANE

Mbalaza wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa kutoka Mkoa wa Mbeya Timida Fyandomo ametembelea eneo la ujenzi wa nyumba ya muhitaji anayejengewa na taasisi ya Tulia Trust katika kata ya Iganjo Mbeya Mjini.

Akiwa katika eneo hilo Timida ameahidi kutoa Godoro kumsaidia muhitaji huyo ikiwa ni kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi wake ambaye ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Spika wa Bunge na  Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson.

Nyumba hiyo inayojengwa kupitia mpango wa Tulia Trust Mtaani Kwatu inatarajiwa kukabidhiwa kwa mlengwa huyo mapema mweezi Aprili mwaka huu.

Kwa upande wake, Ofisa Habari na Mawasiliano wa Taasisi ya Tulia Trust, Joshua Mwakanolo amesema ujenzi wa nyumba hiyo iko katika hatua za mwishoni.

Amesema wanatarajia mara baada ya kukamilisha ujenzi huo uzinduzi utafanywa na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Spika wa Bunge na Mbunge Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson ambaye pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust.

No comments:

Post a Comment