Monday, March 25, 2024

MBUNGE MULUGO AOMBA SERIKALI KUJENGA SOKO LA MADINI

Mbunge wa Jimbo la Songwe Mkoa wa Songwe, Philipo Mulugo ameiomba Serikali kufungua soko la madini katika maeneo ya wachimaji wadogo ili kusaidia usalama mara baada ya kuchimba na kuingizwa sokoni kwa wakati.

Mulugo ametoa ombi hilo kwa Waziri wa Madini, Athon Mavunde aliyefanya ziara Wilaya jimboni kwake na kutoa leseni kwa wachimbaji wadogo 19 kupitia Kikundi cha  Songwe Gold Family (SGF) kutoka  kata ya Saza wilayani humo

“Nipongeze Wizara ya kwa hatua hiyo licha ya Serikali kutoa leseni kuna kila sababu ya kujenga Ofisi ya Madini Wilaya ya Songwe Kata ya Saza ili kuwezesha ukunyaji wa  mapato ya biashara ya madini na  kuepusha utoroshaji

Naye Waziri Athon Mavunde amesema kwa kipindi cha mwaka Julai 2023 mpaka Februari 2024 zaidi ya kilo 729.6 zimeuzwa na kuingiza Sh 101.06 bilioni na utoaji wa leseni hizo itachangia ongezeko la mapato.

Mavunde amesema ili kuboresha wigo mpana katika sekta ya Madini Serikali imetangaza kufuta jumla ya leseni za maombi 2,648 ambazo hazijaendelezwa na kukiuka taratibu za umiliki.

Mwenyekiti wa Umoja wa wachimbaji Wilaya ya Songwe, Simon Ndaki amesema kitendo cha Serikali kuwapa leseni watajikita kuongeza nguvu katika uzalishaji ili kuchangia  mapato ya Serikali

No comments:

Post a Comment