Monday, August 5, 2024

DKT. TULIA AFANIKISHA MATIBABU YA MTOTO MWENYE UVIMBE SHINGONI

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Mbeya Mjini, Dkt. Tulia Ackson,  amefanikisha matibabu ya mtoto Debora Saimon (6) Mkazi wa Kata ya Iganzo Jijini Mbeya aliyekuwa akisumbuliwa na uvimbe shingoni.

Debora amepatiwa matibabu ya kuondoa uvimbe huo katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya ikiwa ni siku chache tangu afikishwe kwa Dkt. Tulia kwa ajili ya kupatiwa msaada wa matibabu.

No comments:

Post a Comment