Tuesday, August 13, 2024

1,000 KUSHIRIKI MASHINDANO YA MAPISHI

 

Taasisi ya Tulia Trust chini ya Mkurugenzi Wake ambaye ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson imeandaa Mashindano ya Mapishi kwa Mama na Baba Lishe  Mbeya Mjini.

Mashindano hayo yanajulikana kama  Tulia Cooking Festival yanatarajiwa kufanyika mwishoni mwa Mwezi Agosti  2024 na  yakishirikisha washiriki 1,000 yenye kauli mbiu isemayo tumia nishati mbadala kuondoa uchafuzi wa mazingira.

Taasisi ya Tulia Trust imekuwa ikifanya matamasha mbalimbali kwa ajili ya kuwapa fursa mbalimbali watanzania ikiwa ni pamoja na kuwainua kiuchumi.


No comments:

Post a Comment