Tuesday, October 29, 2024

WASHINDI TULIA STREET TALENT COMPETITION 2024 KUPELEKWA BAGAMOYO

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Spika wa Bunge na Mbunge Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson amesema walioibuka washindi mashindano ya Tulia Street Talent Competition kuendelezwa kituo cha sanaa na utamaduni Bagamoyo.

Dkt. Tulia amesema Oktoba 27 mwaka huu wakati wa kuhitimisha mashindano hayo huku mgeni rasmi  msanii mkongwe Naseeb Abdul (Diamond Platnam) ambayo yalifanyika kwa siku tatu mfurulizo ikiwa ni msimu wa tano.

"Sisi kama Tulia Trust tunawa andaa na kuibua vipaji ili watakao wahitaji watawatafuta lakini pia niombe Daimond useme neno ili vijana hawa wapone" amesema.

CUoM WAADHIMISHA MIAKA 25 KUMBUKIZI LA MWALIMU NYERERE

Chuo Kikuu Katoriki Mbeya (CUoM) kimefanya kongamano la kumbukizi la miaka 25 ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kama sehemu ya kuenzi mchango wake katika kulitumikia taifa.

Kongamano hilo limefanyika Oktoba 25 mwaka huu huku mgeni rasmi akiwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Makongoro Nyerere lililoshirilisha wadau wakiwepo wanafunzi maprofesa na madaktari kutoka vyuo mbalimbali.

Akizungumza kwenye kongamano hilo Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Rumuald Haule amesema uongozi wa chuo unatambua mchango mkubwa wa hayati Mwalimu Nyerere katika kusimamia sekta ya elimu ya ujamaa na kujitegemea.

Thursday, October 24, 2024

SERIKALI KUTUMIA BILIONI 133.3 KWAAJILI YA KUTOA ELIMU YA FEDHA KWA WAJASILIAMALI WADOGO NA WA KATI

 

Serikali imepanga kutumia kiasi cha Shilingi bilioni 133.310 kwenye sekta ya wajasiriamali wadogo na wa kati kwa kuwawezesha mitaji, kutoa mafunzo ya ujasiriamali, matumizi ya huduma za fedha, tafiti kuhusu sekta ya fedha na kuongeza matumizi ya TEHAMA kwenye sekta ya fedha.

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda amesema hayo jana Jijini Mbeya alipokuwa akifungua Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Kiuchumi” kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, yanayofanyika katika Viwanja vya Ruanda - Nzovwe, jijini Mbeya.
 
 Alisema Serikali imepanga kutekeleza hayo katika Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa 2021/22 - 2025/26 ambapo wahusuka wakuu ni Taasisi za Fedha na watoa huduma za Fedha.
 

CHAUMA YAWAITA VIJANA NA WANAWAKE KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI


Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMA) Mkoa wa Mbeya Ipyana Njiku, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kuchagua viongozi bora wa serikali za mitaa katika uchaguzi utakaofanyika Novemba 27, 2024.

Njiku ametoa rai hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya chama hicho kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa, vitongoji na vijiji utakaofanyika Novemba 27, 2024.

"Tumeona muamko mdogo wa watu kujitokeza kupiga kura lakini niwambie hii ni haki yetu ili kupata viongozi bora kwa maendeleo ya taifa letu", amesema Ipyana Njiku.

Pia Njiku amewataka wananchi kuwa chachu ya kutunza amani ya nchi wakati na baada ya chaguzi ili kuendelea kuwa Taifa moja na kuwaalika wenye nia na uwezo kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali kupitia chama hicho.

"Haki ya kupiga kura ni silaha muhimu kwa kila raia katika kuhakikisha uongozi bora maendeleo yetu, bila kura unatoa nafasi kwa wengine kuamua nani awe kiongozi wao kwahiyo tunaomba siku ya uchaguzi tujitokeze kwa wingi kwenda kuchagua viongozi bora. Pamoja na kupiga kura lakini hii ni fursa kwa watu wenye sifa, dhamira safi, uadilifu na utayari kuwatumikia wananchi kwa kujitokeza kugombea kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma CHAUMMA", amesema Njiku.

DKT. TULIA AGAWA MITUNGI YA GESI KWA MAMANTILIE WA SOKO LA MATOLA

Mbunge wa Mbeya mjini na Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson amegawa mitungi ya nishati gesi bure kwa mamantilie 25 katika soko la  Matola jijini hapa.

Hatua ya Dkt. ambaye ni Rais wa Umoja wa Mabunge Dunia (IPU) kugawa mitungi na nishati safi ya gesi ni kuhamasisha mama lishe kuachana na matumizi ya kuni na mkaa ambayo sio salama kwa afya.

Akizungumza mara baada ya zoezi la kugawa mitungi kwa Mama ntilie 25 amesema hiyo ni sehemu ya ahadi yake lakini pia ni kuunga mkono juhudi za Mh Rais Samia Suluhu Hassan kuhamasisha matumizi ya nishati hiyo.


Wednesday, October 23, 2024

MADIWANI CHUNYA WAMNG'OA MTENDAJI KIJIJI KWA UTORO

Baraza la madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya limemwazimia kumfukuza kazi Ofisa mtendaji wa kijiji cha Matwiga Samweli Koko kwa madai ya kukithiri kwa vitendo vya  ulevi, utoro na matumizi mabaya ya madaraka.

Hatua hiyo imefikiwa jana Oktoba 22, mwaka huu baada ya kikao cha baraza la madiwani cha robo ya tatu kukutana kujadili bajeti ya mwaka wa fedha 2024/25 sambamba na kufanya maamuzi kuhusiana na tuhuma hizo.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chunya, Ramadhan Shumbi amesema wamefikia hatua hiyo kufuatia kukithiri kwa tabia hizo licha ya kumkanya mara kadhaa.

WANANCHI 188,644 WAJIANDIKISHA DAFTARI LA WAPIGA KURA WILAYANI CHUNYA

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya Mubarak Batenga amesema asilimia 89 ya watu 188, 644 wameji andikisha kwenye daftari la wapiga kura na kutarajiwa kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa  Novemba 27 mwaka huu.

Batenga amesema jana Oktoba 22, 2024 wakati akifungua Kikao cha Baraza la Madiwani cha robo ya mwaka 2024/25 cha kujadili taarifa ya fedha na makusanyo ya mapato ya ndani huku wakiwa wamevuka malengo na kufikia Sh 12.5 bilioni.

Amesema kufuatia taarifa ya daftari la wapiga kula madiwani warejee kutoa elimu ya uhamasishaji ili wote waweze kupiga kura kuchagua wenyeviti na wajumbe wa serikali za mitaa ifikapo Novemba 27 Mwaka huu.

Tuesday, October 22, 2024

MEYA ISSA: JIEPUSHENI KUREJEA MIAKA 10 ILIYOPITA


Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya Dourmohamed Issa amewataka wananchi katika Jimbo la Mbeya mjini kutorejea miaka 10 iliyopita kwa kupiga kura kwa viongozi wasiofaa.

Issa amesema jana katika ziara ya Mbunge wa Mbeya Mjini Spika wa Bunge na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Dkt. Tulia Ackson ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwepo elimu na afya katika kata mbalimbali.

Amesema Taifa linaelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na Mkuu 2025 hivyo wananchi wasifanye makosa badala yake wachague viongozi wa CCM akiwepo Mbunge wa Jimbo la Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson na wenyeviti wa serikali za mitaa ambao wataleta tija katika maendeleo.

SPIKA KUCHANGIA SARUJI MIFUKO 200 SHULE YA TAMBUKA RELI


Rais wa umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson amechangia mifuko 200 ya saruji kwa ajili ya ujenzi matundu ya vyoo Shule ya Msingi Tambuka reli.

Dkt. Tulia ametoa ahadi ya mchango huo leo Oktoba 22, 2024 ikiwa ni mwendelezo wa  ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa na matundu ya choo.

Amefikia katika hatua hiyo baada ya kubaini kuwa katika hali mbaya ya uchakavu wa miundombinu sambamba na matundu ya vyoo na majengo ambayo yana hararisha usalama wa wanafunzi.

Monday, October 21, 2024

BITEKO MGENI RASMI WIKI YA HUDUMA ZA FEDHA KITAIFA MBEYA

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Madini Dotto Biteko anatarajia kuwa mgeni rasmi katika maonyesho ya wiki ya huduma za fedha kitaifa ambayo yatafanyika Mkoa wa Mbeya na kuhusisha Taasisi mbalimbali za kifedha.

Maadhimisho hayo yatafunguliwa rasmi kuanzia Oktoba 22 mpaka 26 mwaka huu katika Viwanja vya Ruanda Nzovwe jijini hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 20, 2024 Kamishna msaidizi wa Idara ya Uendeshaji sekta ya fedha kutoka wizarani Janeth Hiza amesema lengo ni kutekeleza mpango mkuu wa maendeleo ya sekta hiyo kwa mwaka 2020/21 na 2029/30.

DKT. TULIA AFANYA ZIARA KUKAGUA MIRADI YA ELIMU AFYA JIJI LA MBEYA

Spika wa Bunge na Mbunge Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson amefanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na fedha za serikali kuu ,mapato ya ndani ya Halmashauri na mfuko wa jimbo.

Katika ziara yake Dkt. Tulia ameambatana na Mkurugenzi wa Jiji John Nchimbi, Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya Dourmohamed Issa wakiwepo madiwani na watendaji wengine wa serikali.

Dkt. Tulia ambaye  ni Rais ya Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) ameeleza malengo ya ziara yake ni kukagua utekelezaji wa miradi ya sekta ya elimu na afya sambamba na ujenzi bweni na wanafunzi wenye mahitaji maalum ya katika Shule ya Mwenge lenye uwezo wa kuchukua watu 200.

Wednesday, October 16, 2024

MILIONI 15 KUTUMIKA UJENZI SOKO LA MBOGA MBOGA KATA YA ISANGA

Halmashauri ya Jiji la Mbeya imeanza utekelezaji wa Ujenzi wa mradi wa soko la kisasa la  mbogamboga katika Kata ya Isanga.

Mradi huo kwa awamu ya kwanza umegharimu Tsh. 15 milioni na litakapo kamilika litakuwa fursa kwa wakulima wa mbogamboga kujikwamua kiuchumu na kuongeza wigo wa masoko ya ndani na nje.

Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya Dourmohamed Issa amesema leo Oktoba 16 mwaka huu na kwamba ujenzi wa soko hilo ni sehemu ya miradi ambayo imepokelewa katika Kata ya Isanga.

"Ujenzi wa soko la mbogamboga la Isanga utekelezaji wake umeanza na uko katika hatua nzuri sambamba na miradi mingine ya uboreshwaji wa barabara na kufunga taa" amesema Issa.

Tuesday, October 15, 2024

MBUNGE WA LUPA ALIA NA TRA UTITIRI WA KODI WACHIMBAJI WADOGO

Mbunge wa Lupa Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya, Masache Kasaka ameiomba serikali kuangalia uwezekano wa kupunguza utitiri wa tozo kwa wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu.

Masache amesema Oktoka 14 ikiwa ni usiku wa madini ambayo Mkoa wa Mkuu wa Mkoa Juma Homera alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Waziri wa Madini Athon Mavunde.

"Tukuombe Mkuu wa Mkoa tuwasilishie kilio chetu kwa Waziri mwenye dhamana kutazama changamoto ya cha utitiri wa tozo kwa wachimbaji wadogo ili kuwezesha kuendesha shughuli zao na kutokwepa kulipa kodi" ameseme Masache.

RAIS WA UTPC AKIJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA


Rais wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) Deogratius Nsokolo, amejiandikisha katika daftari la wakazi katika kitongoji cha Kabatini kijiji cha Isinde katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba 27 mwaka huu.


Nsokolo ametoa wito kwa waandishi wa habari nchini kuendelea kuhamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha ili waweze kuchagua viongozi wanaowataka watakaosaidia kuleta maendeleo katika maeneo yao.

MEYA MBEYA AHAMASISHA WANANCHI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA


Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya Dourmohamed Issa amehamasisha wananchi na vyama vya siasa kusimamisha wagombea kushiriki kikamilifu kwenye mchakato wa uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024.

Issa ambaye ni Diwani wa Kata ya Isanga mesema leo Oktoba 14, 2024 mara baada ya kujiandikisha kwenye Daftari la Wapigakura kwenye mtaa wa Ilolo Kata ya Isanga Jijini hapa.

Amesema kuwa ni wajibu wa vyama vya siasa kuhamasisha wananchi kushiriki kuanzia zoezi la uchaguzi wa serikali za mitaa kuanzia hatua uandikishaji katika dafrari la wapigakura.

Thursday, October 10, 2024

AGRICON BORESHA CHAI YANUFAISHA WAKULIMA MBEYA, NJOMBE, IRINGA

 

Wakulima zaidi ya  22,000 Mikoa ya Mbeya,Njombe na Iringa wamenufaika na  mafunzo ya shamba darasa kupitia mradi  Agricon Boresha  Chai uliotekelezwa na Shirika la IDH Tanzania kwa ufadhiri wa Jumuiya ya Ulaya (EU)

Meneja mradi wa Shirika hilo  ,Elikinda Tenga amesema  jana Oktoba 9,2924  wakati  wa  Mahafari ya  Mafunzo ya  Wakulima ya Shamba  Darasa(FFS)  yaliyofanyika katika kijiji cha Syukula Kata ya Kyimo Wilaya ya Rungwe

Amesema  mradi wa Agricon Boresha chai umelenga kuwajengea uwezo wakulima na kuwezesha upatikanaji wa  vifaa vya kisasa na matumizi ya teknolojia kutumia matone kunyunyiza kwenye mashamba.

MAWAKALA VYAMA VYA SIASA WAAPISHWA JIJI lA MBEYA

Halmashauri ya Jiji la Mbeya limewaapisha mawakala wa vyama vya siasa leo  Oktoba 10, 2024 katika ukumbi wa Mkapa Jijini hapa.

Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbeya Teddy Mlimba amewaapisha mawakala hao huku  viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa wakishiriki na kutoa maoni yao kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba 27, 2024.

Ofisa uchaguzi Jiji la Mbeya Gregory Emmanuel amesema uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu utakuwa wa huru na kuzingatia demokrasia ya mifumo ya vyama vingi.

Tuesday, October 8, 2024

WASIMAMIZI WA UCHAGUZI WAAPISHWA WAONYWA MATUMIZI YA POMBE

 Halmashauri ya Jiji la Mbeya leo Oktoba 8, 2024 imefanya zoezi la kuwaapisha wasimamizi wa uchaguzi zaidi ya 200 ngazi za mitaa katika kuelekea zoezi la uandikishaji wananchi kwenye daftari la kudumu la wapigaku.

Zoezi hilo limefanyika katika Ukumbi wa Mkapa Jijini hapa kwa  kula kiapo mbele ya Hakimu wa Mahakama wa Wilaya Mkoa wa Mbeya .

Awali akizungumza baada ya kuapishwa, Msimamizi msaidizi wa uchaguzi Jiji la Mbeya Oddo Nduguru amewaonya wasimamizi kuepuka matumizi ya vilevi wakati wa kuendesha zoezi hilo ili kutunza siri za kiapo walichopewa.

"Tunaelekea zoezi la Uandikishaji Daftari la kudumu la wapigakura litakaloanza Oktoba 11 mpaka 20 mwaka huu kwa wale wanatumia vilevi tunaomba wakawe wavumilivu kwa siku 10 za kuendesha zoezi hilo" amesema.

UJENZI MRADI WA MAJI MTO KIWIRA WAFIKIA ASILIMIA 35

Utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa kimkakati wa Maji kutoka chanzo cha Mto Kiwira Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya umefikia asilimia 35 ambao unatarajia kunufaisha watu zaidi milioni 1.4.

Mkurugenzi uzalishaji na usambazaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya (Mbeya (MBEYA - UWSA) Mhandisi Barnabas Konga amesema jana wakati akitoa taarifa kwa Waziri wa Sheria na Katiba Prof. Palamagamba Kapudi.

Mradi huo utajengwa kwa miaka miwili ambapo ukikamilika utazalisha lita milioni 184 kwa siku na wananchi zaidi ya milioni 1.4 katika Mkoa wa Mbeya na Mji wa Mbalizi watanufaika kwa kipindi cha miaka 20 ijayo.

Monday, October 7, 2024

PROF. KABUDI AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI WA BILIONI 4.8 MBEYA

Waziri wa Sheria na Katiba Prof. Palamagamba Kabudi ameweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji kutoka chanzo cha Mto Ilungu Kata ya Utengule Usongwe Wilaya ya Mbeya.

Mradi huo una thamani ya zaidi ya Sh 4.8 bilioni na kutekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya (Mbeya-UWSA) ambao unatarajia kunufaisha wananchi 110,000 kutoka vijiji vitatu na kata nne.

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Ihango kata ya Utengule Usongwe Prof. Kabudi ameeleza dhamira ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuona wananchi wanaondokana na changamoto ya maji.

"Nipongeze sana Mamlaka ya Maji Mbeya kwa kutekeleza mradi huu mkubwa ambao unakwenda kuwa mwarobaini kwa wananchi kupata huduma ya maji safi na salama kwa wakati" amesema Prof. Kabudi.

Friday, October 4, 2024

NCHIMBI AWATAKA VIONGOZI WA DINI KUHAMASISHA WAUMINI KUPIGA KURA

Msimamizi wa Uchaguzi Mdogo wa Serikali za mitaa Jiji la Mbeya John Nchimbi amewaomba viongozi wa dini,machifu kuhamasisha wananchi kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura na kushiriki  katika uchaguzi Novemba 27, 2024 kuchagua viongozi bora.

Nchimbi amesema leo Ijumaa Oktoba 4, 2024 kwenye kikao kilichohusisha viongozi wa dini,machifu wadau na viongozi wa vyama siasa kilicholenga kutoa maelekezo kuelekea uchaguzi mdogo wa serikali za mitaa.

Nchimbi amesema kuwa mchakato wa kuelekea uchaguzi umekamilika hivyo wananchi wajitokeze kushiriki kikamilifu hususani kujiandisha katika Daftari la kudumu la wapiga kura ikiwa ni wajibu wao wa kikatiba.

Thursday, October 3, 2024

MEYA ISSA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA TACTIC

Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya Dourmohamed Issa leo amefanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya Soko la Kisasa la Matola  na mitaro ya kutililisha Maji ya Mvua  katika Kata ya Nzovwe.

Miradi hiyo inatekelezwa kupitia Mradi wa kuboresha majiji (TACTIC) ambayo iko katika hatua nzuri za utekelezaji.


Akizungumza na Mwandishi wa habari leo mara baada ya kufanya ziara hiyo, Issa ameipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Sami Suluhu Hassan kwa kuleta miradi mikubwa ya kimkakati Jijini hapa.

"Kipindi cha miaka mitatu ya Rais Samia Suluhu Hassan na Mbunge wa Mbeya mjini, Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson wanaona Mkoa wa Mbeya unakwenda kasi katika miradi ya maendeleo" amesema Issa.


Amesema amekuwa Meya wa IPU kwani miradi inatekelezwa kwa kasi ukiachia ujenzi wa soko na mifereji pia kuna ujenzi wa kituo kikubwa cha kisasa cha mabasi ya mikoani ambacho kitakuwa chachu ya fursa za kiuchumi na mwingiliano wa shughuli za kiuchumi.

MKUTANO WA MWAKA WA WAKUU WA MAMLAKA ZA KUPAMBANA NA RUSHWA KWA NCHI ZA SADC 2024 - LUSAKA, ZAMBIA

Wakati Dunia ikishuhudia majanga katika maeneo mbalimbali, Mamlaka za Kupambana na Rushwa ukanda wa SADC zimetahadharishwa kuwa makini kwani mikakati ya haraka inayoandaliwa kukabiliana na hali hiyo inaweza kutoa mianya ya rushwa.
 
Akizungumza Oktoba 2, 2024 katika hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Wakuu wa mamlaka hizo jijini Lusaka - Zambia, Mwenyekiti mpya wa Kamati ya SADC ya Kupambana na Rushwa (SADC Anti Corruption Committee - SACC) ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini - TAKUKURU, Crispin Francis Chalamila, amefafanua kuwa hatari ya uwepo wa vitendo vya rushwa inaweza kujitokeza wakati wa mchakato wa kupata na au kutoa misaada wakati wa dharura. 

“Hatua zote za mnyororo wa utoaji wa misaada ziko katika hatari ya rushwa kutokana na dharura inayokuwepo", alisema.


Wakuu wa Mamlaka za Kupambana na Rushwa ukanda wa SADC pamoja na Viongozi na wajumbe mbalimbali kutoka katika mamlaka hizo za Nchi 14 wanachama waliohudhuria mkutano huo.

Tuesday, October 1, 2024

MBUNGE MASACHE AZINDUA MASHINDANO AMBWENE CUP

Mbunge wa Jimbo la Lupa Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya Masache Kasaka amezindua mashindano ya Ambene Cup 2024 yanayotimua kivumbi katika viwanja vya Matundasi "A".

Mashindano hayo yatashirikisha timu 32 huku yakifunguliwa na timu ya Chokaa FC na kisimani FC zote za wilayani Chunya katika kipindi cha kwanza cha mchezo.

Imeelezwa timu zitakazo ibuka kidedea zitajinyakulia kitita cha fedha huku  mbalimba mshindi wa kwanza  Sh 5 milioni wa pili Sh 3 milioni wa tatu Sh 2 milioni huku wa nne shilingi milioni moja.

Akizungumza mara baada ya kuzindua mashindano hayo Masache ametaka ukawe wa haki bila kupendelea upande wowote na vijana kutumia kama fursa ya ajira na kiuchumi.


BODOBODA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA BARABARANI

Mbunge Jimbo la Mbeya Mjini ambaye ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Dkt. Tulia Ackson amezindua Jengo la Ofisi ya Bodaboda Kanda ya Soweto Mbeya Mjini huku akisisitiza kutii sheria za usalama barabarani.

Ofisi hiyo imejengwa katika Mtaa wa James Kata ya Ilemi kwa Jitihada za Wanachama wa Bodaboda Kanda ya Soweto ili iwasaidie katika Shughuli mbalimbali za Kiofisi na kuwaongezea kipato kupitia Vyumba vya Biashara vilivyojengwa kwenye Ofisi hiyo.

Dkt. Tulia amewaasa Madereva Bodaboda kufuata Sheria za Usalama Barabarani na kutumia vizuri vyombo vyao vya Moto katika kujitafutia kipato na sio uhalifu ili kutimiza Malengo yao kama ambavyo wamefanikisha kujenga Ofisi hiyo.

Aidha Dkt. Tulia amewataka Wananchi  wajitokeza kujiandisha kwenye Daftari la Mpiga Kura ili waweze kutimiza haki yao ya kupiga kura kuwachagua Viongozi wa Serikali za Mitaa katika Uchaguzi Utakaofanyika Mwezi Oktoba Mwaka huu.


DKT. TULIA ACHANGIA MIFUKO 100 YA SARUJI KWAAJILI YA UJENZI WA OFISI YA SERIKALI YA MTAA

Spika wa Bunge na Mbunge Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson amechangia mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya serikali ya Mtaa Kata ya Isanga Jijini hapa.

Mbali na kuchangia ujenzi huo pia amefanya ziara ya kukagua ujenzi wa zahanati ya kata hiyo sambamba na  kufungua ofisi ya bodaboda  eneo la Ilemi Jijini hapa.

Akizungumza na mamia ya wananchi leo Oktoba mosi Dkt. Tulia amesema kuwa serikali itaendelea kuboresha miradi ya maendeleo kama kutekeleza ilani ya uchaguzi 2024/25.

Amesema pia serikali imewekeza zaidi ya Sh 11 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Mama na Mtoto katika Hosptali ya Rufaa Kanda kitengo cha Wazazi Meta.

Naye Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya na Diwani wa kata ya Isanga Dour mohamed Issa amesema  kwa kipindi cha uongozi wa  Dkt. Tulia wamepata miradi mbalimbali kama miundombinu ya barabara, zahanati.

"Tuna kila sababu ya kujivunia uwepo wa Mbunge Dkt. Tulia tumepokea miradi mbalimbali ambayo imekuwa mwarobaini na tija kubwa kwa  wananchi".


Mkazi wa Isanga Stella Joel ameomba serikali kuharakishwa ujenzi wa zahanati ya kata ili kuokoa wakinamama wajawazito kutembea umbali mrefu kufuata huduma.