Monday, July 29, 2024

WANANCHI ISYESYE WAMSHUKURU DKT. TULIA KUGUSA WAHITAJI

Wananchi kata ya Isyesye jijini Mbeya wamesema kitendo cha Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Dkt. Tulia Ackson kusaidia wahitaji akiwepo mtoto kwenye ulemavu Jane Ambilikile (13) ni kujishusha kwa wananchi wasiojiweza.

Kauli hiyo wameitoa jana kwa nyakati tofauti mara baada ya kukabidhi nyumba mbili za wahitaji kwa familia ya Familia ya Damiani Mbwiga (50) na baiskeli mbili kwa walemavu akiwepo Mtoto Janeth Ambilikile (13) vilivyotolewa kupitia Taasisi ya Tulia Trust.

Akizungumza kwa niaba ya Wananchi Tabu Joel amesema kwa nafasi yake ya juu licha ya ubunge amekuwa ni kiongozi wa kipeke anawafuta machozi wanyonge wasio jiweza tofauti jamii inayo wazunguka.


Friday, July 26, 2024

KITUO CHA MIONZI KUJENGWA JIJINI MBEYA

Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kwa kushirikiana na Taasisi ya Saratani (Ocean Road) wanatajia kujenga kituo cha mionzi na kusimika mashine za kisasa.

Mkurugenzi mtendaji wa Hosptali ya Rufaa Kanda Dkt. Godlove Mbwanji amesema mara baada ya kutembelea kitengo cha huduma za mifumo ya chakula hosptalini hapo na kuona huduma mbalimbali za kitabibu zinazotolewa.

Amesema kitendo cha Serikali kubariki ushirikiano wa Taasisi ya Saratani Ocen Road Hosptali ya Rufaa Kanda kusimika mashine za mionzi utasaidia kuwapunguzia gharama wagonjwa kusafiri umbali mrefu kufuata huduma.

Wednesday, July 24, 2024

TANZANIA KUNUFAIKA NA MAFUNZO NCHINI INDIA

Bunge la India limeahidi kutoa fursa zaidi za mafunzo ya kuwajengea uwezo Watumishi wa umma kupitia Taasisi yake ya Utafiti na Mafunzo ya Kidemokrasia (PRIDE) inayoendeshwa na Bunge hilo.

Ahadi hiyo imetolewa jana Julai 23, 2024 na Spika wa Bunge la India (Lok Sabha), Om Birla wakati wa mazungumzo yake na Spika wa Bunge la Tanzania ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Dkt. Tulia Ackson katika Ofisi za Bunge hilo Jijini New Delhi.

Katika mazungumzo hayo pamoja na mambo mengine, Birla amemuelezea Dkt. Tulia kuhusu maboresho yaliyofanywa na Taasisi hiyo ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya ufadhili kwa Watumishi wa umma kutoka nchini mbalimbali Duniani hususani wabunge na watumishi wa Mabunge ya nchi hizo.

 

MZRH KUBORESHA MIUNDOMBINU YA MAKUNDI MAALUM


Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya imesema itaendelea kuboresha miundombinu  rafiki ya huduma za  afya hususani upasuaji na macho kwa makundi maalum wakiwepo watu wenye  walemavu wa kusikia (viziwi).

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi mtendaji wa Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya (MZRH) Dkt. Godlove Mbwanji wakati akifunga mkutano ulioandaliwa na Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) Mkoa wa Mbeya.

Dkt. Mbwanji amesema katika kuhakikisha huduma bora za afya zinaboreshwa  kwa makundi maalum Hosptali ya Kanda imekuwa ya kwanza kuwa na mkalimani wa lugha ya alama ili waweze kupatiwa huduma rafiki za afya.

Tuesday, July 23, 2024

DCEA AONYA MADEREVA KUJIHUSISHA USAFIRISHAJI DAWA ZA KULEVYA

Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti  na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Aretas Lyimo ameonya madereva na makondakta  mabasi ya abiria  kujiepusha na tabia ya kusafirisha dawa za kulevya wakibainika hatua za kisheria zitachukuliwa na vyombo vya moto kutaifishwa.

Kamishna Jenerali, Aretas Lyimo amesema hayo mkoani Mbeya kwenye mkutano uluihusisha Kamati za Ulinzi na Usalama, wadau wa sekta ya afya na walaibu wa dawa za kulevya uliolenga uhamasishaji mapambano ya dawa za kulevya uliofadhiriwa na shirika la HJFMRI.

Amesema kwa sasa serikali imefanya mabadiliko ya sheria ya usafirishaji wa dawa za kulevya kwa kutaifisha vyombo vya moto na madereva na makondakta stahiki.

DKT. TULIA ADHURU KABURI LA BABA WA TAIFA WA INDIA

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 23 Julai, 2024 ametembelea na kuweka shada la maua kwenye makumbusho ya kaburi la Baba wa Taifa la India hayati Mahatma Gandhi yaliyopo Jijini New Delhi, India.

Monday, July 22, 2024

TAMASHA NGOMA ZA ASILI MSIMU WA NANE KUTIMUA KIVUMBI SEPTEMBA 2024

Taasisi ya Tulia Trust imeandaa Tamasha la ngoma za asili laa makabila mbalimbali ya asili  msimu wa nane litalofanyika septemba mwaka huu.

Tamasha hill litashirikisha washiriki kutoka Tanzania bara na viziwani lengo ni  kuenzi tamaduni na kuonyesha uhalisia wa makabila

Ofisa habari na mawasiliano wa Taasisi ya Tulia Trust, Joshua Mwakanolo amesema leo Jumatatu Julai 22, 2024 na kwamba tamasha hilo litafanyika kuanzia Septemba 26 mpaka 28 mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa zamani uliopo kata ya Iyela Jijini hapa.

TULIA TRUST YAMSAIDIA KIJANA ALIYESHINDWA KUJIUNGA NA KIDATAO CHA TANO KWA KUKOSA MAHITAJI

Taasisi ya Tulia Trust imetoa tabasamu kwa Mussa Mwashilindi (17) akiyekwama kujiunga kidato cha tano kwa kukosa mahitaji ikiwepo sare za shule, daftari na mengineyo.

Mussa ambaye anaishi dada yake na wadogo zake wawili baada ya mama yao mzazi kufariki ghafla na kuwaacha wakijitegemea wenyewe kuendesha maisha.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi mahitaji hayo, ofisa habari kutoka Idara ya habari taasisi ya Tulia Trust Addy Kalinjila amesema mwanafunzi huyo alichaguliwa kujiunga kidato cha tano shule ya sekondari ya Dkt. Tulia iliyopo Kata ya Itende Mbeya Mjini.

Thursday, July 18, 2024

HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA YAWEKA ALAMA MUHIMU KILELE CHA MLIMA KILIMANJARO

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya kanda Mbeya wameendelea kuipongeza Serikali staili ya kipekee kwa kuboresha huduma za afya nchi katika kuwa hudumia wananchi, pia kuiunga mkono Serikali kufanya utalii wa ndani kwa vitendo kama alivyofanya Rais Dkt. Samia kwenye Filamu ya The Royal Tour.

Akiongea juu  kilele cha Mlima Kilimanjaro kwa niaba Watumishi wa hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, Salum Msambaji ameleza kuwa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imetumia njia hiyo pia kuishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji wa zaidi ya Bilioni 26 katika kuboresha Miundombinu, vifaa tiba, na mashine katika Hospitali Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya pamoja na huduma za kibingwa na bingwa bobezi.

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya wameushukuru Uongozi wa Waziri Ummy Mwalimu (Mb) na wasaidizi wake wa Wizara ya Afya kwa ushirikiano na maelekezo mazuri wanaopatiwa ambapo yamesaidia utendaji kazi mzuri katika kuwahudumia wananchi wa Nyanda za Juu Kusini na nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika SADC zikiwemo Zambia na Malawi.

Vilevile, Salumu ameeleza kuwa nia nyingine ya watumishi wa hospitali ya rufaa ya kanda Mbeya kupandisa bendera hiyo ya MZRH ni pamoja na kuitangaza Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Kitaifa na Kimataifa kutokana na  Mlima Kilimanjaro kuwa ni mojawapo ya alama ya Taifa, kuwa ni mlima mrefu zaidi barani.

Monday, July 15, 2024

TANROADS MBIONI KUANZA UJENZI BARABARA YA MBALIZI - SHIGAMBA

Wakala wa barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Mbeya umesema unatarajia kuanza ujenzi wa barabara kwa kiwango cha rami kutoka Mbalizi hadi Shigamba na Umalila baada ya serikali kutoa bilioni 2.

Kaimu Meneja, TANROADS Mkoa wa Mbeya Mhandisi, Kamokene Sanke amesema leo Jumamosi Julai 13, 2024 wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Sanje kata ya Santilya wilayani Mbeya kwenye ziara ya Mbunge wa Mbeya vijijini Oran Manasse Njeza ya kusikiliza kero za wananchi.

Amesema Serikali Kuu chini Rais Samia Suluhu Hassan imetoa Sh 2 bilioni  kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hizo kwa kiwango cha rami kutoka Mbalizi mpaka Shigamba yenye urefu wa Km 52 ambayo inatarajia kuanza hivi karibuni.

Friday, July 12, 2024

MGANGA WA KIENYEJI MATATANI KWA KUZINI NA MAHARIM

Masumbuko Wenson Sompo (51) Mkazi wa Sangambi Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya amefikishwa Mahakama ya Wilaya kwa tuhuma za kuzini na maharim.

Akisoma hati ya mashitaka kesi ya jinai namba 19278/ 2024 Kaihwa Stephen Mayanja mbele ya Hakimu wa Wilaya ya Chunya James Mhanusi amesema mtuhumiwa alitenda kosa hilo juni 23, 2024 porini majira ya saa tisa usiku.

Mayanja amesema kosa hilo ni kinyume cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai kifungu cha 158 (1) (a) cha kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2022 ambapo mshitakiwa amekana kutenda kosa.

TULIA TRAST YAMPA TABASAMU MWANAFUNZI ELIMU YA SEKONDARI

Mwanafunzi wa kidato cha pili shule ya Sekondari Itagano Jijini Mbeya  Sikujua Dickson (16) amemuomba Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson kumsaidia ili atimize ndoto yake  kupata elimu kufuatia Mama yake mzazi kuficha sare za shule na kumfanyia vitendo vya ukatili.

Sikujua amesema leo Ijumaa Julai 12, 2024 Mara baada ya Taasisi ya Tulia Trust kumkabidhi mahitaji mbalimbali ikiwepo viatu, sare za shule sambamba na kumuondoa nyumbani kwa wazazi wake  kumuendeleza kielimu .

Sikujua amefikia kutoa ombi hilo baada ya kuchoshwa na tabia ya Mama yake mzazi kuficha sare za shule kwa lengo la kumkatisha masomo hali ambayo amesema apendezwi nayo.

NDELE MWASELELA AKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO MBEYA DC

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa (MNEC) Ndele Mwaselela amekabidhi vifaa vya michezo kwa timu 16 bora zinazoshiriki ligi ya Mama Samia Mshikamano Cup inayoendelea katika viunga vya wilaya hiyo, vifaa hivyo ni pamoja na mipira na jezi.

Mwaselela amekabidhi vifaa hivyo vya michezo kwa timu 16 Julai 11, 2024 katika ofisi za CCM mkoa wa Mbeya.

Hata hivyo Mwaselela amesema kuwa michezo ikawe chombo cha kuzitafsiri 4R za Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na kuelezwa kwa mambo makubwa yaliyofanywa na Rais Samia katika kipindi cha uongozi wake.

DKT. TULIA NA RAIS WA URUSI WAJADILI NAMNA BORA YA KUIMARISHA AMANI DUNIANI

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson,  amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Urusi, Vladimir Putin Jijini St. Petersburg nchini Urusi leo Julai 12, 2024 ambapo katika mazungumzo yao wamejadili kuhusu namna bora ya kuimarisha amani Duniani.

“Kabla ya kuzungumza naye tayari tulishazungumza na Maspika wa nchi zote hizo mbili na sisi kama Umoja wa Mabunge Duniani tumezungumza naye kama Kiongozi wa nchi katika sura ambayo tunaweza kuziweka pamoja nchi zote mbili na tutarajie kwamba IPU itatengeneza fursa ya Mabunge ya pande zote ili kuweza kuzungumzia amani katika maeneo yao ya utawala” amesema Dkt. Tulia.


TULIA TRUST YATOA MSAADA WA TAULO ZA KIKE MASHULENI

Taasisi ya Tulia Trust imeanza zoezi la ugawaji na utoaji elimu ya matumizi yaTaulo za kike wenye mahitaji maalumu kwa shule za sekondari kata 36 za Jiji la Mbeya.

Lengo ni kuwezesha wanafunzi wa kike kutoka mazingira magumu kuweza kupata elimu bora pasipo kuwa na changamoto zinazotokana na hedhi.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa zoezi hilo, Meneja wa Taasisi ya Tulia Trust, Jackline Boaz amesema watazifikia kata tano Mbeya mjini kwa kutoa taulo za kike.

Amesema zoezi hilo litanufaisha kwa wanafunzi wa kike kutoka kaya maskini ambao wamepewa taulo za kike 550 sambamba na viatu pea 50.

Thursday, July 11, 2024

MAFUNZO YA MFUMO WA GAMIS YATOLEWA KWA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA


Menejimenti ya hospitali, wakiwemo watendaji kutoka Idara  mbalimbali za Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH) leo Julai 11, 2024 wamepewa mafunzo ya Mfumo wa Usimamizi wa Mali za Serikali (Government Assets Management Information System (GAMIS) ili kuwawezesha kuingiza na kuhuisha taarifa za mali za taasisi kwenye mfumo kwa wakati.

Mafunzo hayo yametolewa na wakufunzi kutoka Wizara ya Fedha Said Mtatura na Simon Njoka ambaye pia ni msimamizi wa mali za Serikali Mkoa wa Mbeya na Songwe na kueleza kuwa mafunzo hayo ni wezeshi kwa maafisa usimamizi wa mali za Serikali hususani maafisa wapya kwa lengo la kuwajengea uwezo kwenye matumizi ya moduli zilizopo kwenye Mfumo wa GAMIS.

DKT. TULIA AJITOLEA KUMSOMESHA MTOTO ALIESHINDWA KUENDELEA NA MASOMO KWA KUKOSA MAHITAJI

Kijana Richard (kushoto) akiagana na Mratibu wa Tulia Trust Addy Kalinjila Mara baada ya kumkabidhi kwa uongozi wa shule ya wavulana Uwata.

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani, (IPU) Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson amejitolea kukuendeleza elimu ya kidato cha tano na sita Yatima Shadrack Mwaisela (17) aliyekwama kuendelea na masomo kwa kukosa mahitaji.

Kijana Richard aliyekuwa akiishi na bibi yake mkazi wa kijiji cha Kisondela Wilaya ya Rungwe  amekabidhiwa leo Alhamisi  kwa uongozi wa Shule ya Sekondari ya wavulana Uwata kupitia Taasisi ya Tulia Trust.

Akizungumza mara baada ya kumpokea Mwanafunzi huyo Makamu Mkuu wa Shule Wavulana  Uwata, Marco Mwakanyamale amemshukuru Dkt. Tulia kwa moyo wa kumuendeleza  kielimu kufatiatia kutoka katika mazingira magumu.

RUNGWE KUTUMIA NGOMA ZA ASILI KUTANGAZA UTALII

Mbunge wa Jimbo la Rungwe, Athon Mwantona ameanzisha mashindano ya ngoma za asili,nyimbo za injili na mashindano ya mpira wa miguu kwa lengo la kutangaza fursa za uwekezaji kwenye utalii.

 Katibu wa Mbunge, Gabriel Mwakagenda amesema leo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mipango mikakati ya kuitangaza Wilaya ya Rungwe na kuvutia uwekezaji.

Mwakagenda amesema Wilaya ya Rungwe ina vivutio vingi vya utalii ambavyo vikitumika vinatengeneza fursa za kiuchumi kwa vijana na hata mapato kwa serikali.

Wednesday, July 10, 2024

BILION 5.3 KUJENGA SOKO LA KISASA LA NDIZI RUNGWE

Serikali  Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya inatarajia kutumia zaidi ya Sh 5.3 bilioni kwa ajili ya  ujenzi wa soko la kisasa la mazao ikiwepo ndizi na parachichi.

Hatua hiyo imekuja kufuatia kuwepo kwa changamoto ya masoko ya uhakika hali iliyopelekea wakulima kushindwa kunufaika na uzalishaji

Kauli hiyo imetolewa leo Jumatano Julai 10, 2024 na katibu wa Mbunge wa Jimbo la Rungwe, Gabriel Mwakagenda kwa niaba ya Mbunge Athon Mwakagenda.

Amesema kuwa mradi huo wa soko la kisasa itakuwepo miundombinu mbalimbali ikiwepo migahawa,maegesho,Taasisi za kifedha za kitanzania na kigeni na huduma nyinginezo.

Tuesday, July 9, 2024

DC: MALISA ATAKA WATU WENYE UALBINO WALINDWE


Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Beno Malisa ameagiza viongozi wa serikali za mitaa kuchukua hatua ya kuelimisha jamii kuwalinda watu wenye ualbino.

Malisa amesema leo Jumatatu Julai 8, 2024 kwenye maadhimisho ya siku ya afya ya ngozi duniani iliyofanyika kitaifa Mkoa wa Mbeya na kuratibiwa na Shirika la Standing Voice kwa kushirikiana na Hosptali ya Rufaa ya Mkoa.

Amesema sasa imefika mwisho kwa watu ambao wanatafuta mali kwa kuwaua albino na kisha kwenda kuuza viungo vyao watakao bainika sheria itachukua mkondo wake.

Friday, July 5, 2024

DKT. TULIA AMGUSA YATIMA KUCHANGIA MAHITAJI YA SHULE

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU ) Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson ametoa zaidi ya Sh 500,000 kwa ajili ya mahitaji ya shule kwa  mtoto yatima aliyechaguliwa kujiunga kidato cha tano Shule ya Sekondari Isongole Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya.

Fedha hizo zimekabidhiwa leo Ijumaa Julai 5, 2024 na Ofisa habari na Mawasilino wa Taasisi ya Tulia Trust Addy Kalinjila kwa mlemavu Richard Mwaisela (18) ambaye ni yatima anayelelewa na bibi yake  ambaye alikwama kuendelea na masomo kwa kukosa mahitaji.

"Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust ameguswa kumsaidia Richard aweze kutimiza ndoto yake ya kupata elimu kwani bibi yake mkazi wa kijiji cha Mpuga kata ya Kisondela  alikosa uwezo wa kumsaidia baada ya kufaulu kujiunga idato cha tano Shule ya Sekondari ya Isongole na kushindwa  kuanza masomo " amesema Kalinjila.

Kalinjila amesema kuwa kama Taasisi wataendelea kuigusa jamii yenye mahitaji kwa kuchangia sekta ya elimu, afya na kuwezesha jamii isiyojiweza.

Kwa upande wake kijana Richard amemshukuru Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) kwa kumuwezesha kupata mahitaji na kuhaidi kusoma kwa bidhii ili kutimiza ndoto zake za kupata elimu.

Thursday, July 4, 2024

ALIYECHOMA PICHA YA RAIS AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA MIWILI


Mahakama ya hakimu mkazi wilaya ya Rungwe mkoa wa Mbeya imemtia hatiani ni kumhukumu kutumikia kifungo cha miaka miwili Shadrack Chaula (24) au kulipa faini ya Shilingi milioni tano.

Shadrack ametiwa hatiani kwa kosa la kusambaza taarifa za uongo kupitia mtandao wa kijamii wa Tik Tok kinyume cha  kifungu cha sheria 16 ya mtandao ya kijamii.

Hukumu hiyo imesomwa leo Julai 4, 2024 na Hakimu mkazi Mkuu wa Mahakama ya Wilaya ya Rungwe, Shamla Shehagiro baada ya mawakili wawili wa serikali, Rosemary Mginyi na Veronica Mtafya kutoa ushahidi mahakamani hapo.

Imeelezwa mahakamani hapo mtuhumiwa alitenda kosa hilo June 22 mwaka huu katika eneo la Ntokela wilaya ya Rungwe kwa kusambaza video yenye taarifa za uongo kinyume cha kifungu cha sheria 16 ya makosa ya mitandao.


TAASISI YA TULIA TRUST IMETOA BANDO TISA ZA BATI UJENZI WA UKUMBI

Taasisis ya Tulia Trust umekabidhi msaada wa mabati bando tisa za bati kwa ajili ya ujenzi wa ukumbi wa  ofisi ya chama cha Mapinduzi shina namba nane kata ya Iyela Jijini hapa.

Msaada huo wa Mabati umetolewa na Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Mbeya mjini Spika wa Bunge na Rais wa Umoja wa Mabunge (IPU) Dkt. Tulia Ackso Ackson, Steven Chambanenge.

Amesema kuwa Dkt. Tulia amekuwa na mapenzi mema kwa wanambeya na kuwataka asifanye makosa unapofika wakati kwa kupiga kura za kishindo kwa Rais Samia Suluhu Hassan na Mbunge wao Dkt. Tulia Ackson.


Kwa upande wake Mjumbe wa shina namba nane, Gaporic Lwibha amesema anamshukuru Mbunge wa Jimbo la Mbeya mjini na Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson kwa kuchangia ujenzi wa ukumbi huo.

"Ndugu zangu tulitumia muda mfupi sana kuomba lakini leo hii tumekabidhiwa, naomba Katibu wa Mbunge nifikishie salama za shukrani zetu kuna majibu yake 2025 kwake Rais Samia Suluhu Hassan" amesema.

Monday, July 1, 2024

KATA 13 JIJI LA MBEYA ZANUFAIKA NA MICHE YA PARACHICHI 1,120 BURE

Miche zaidi ya 1,120 ya matunda aina ya parachichi kwa wananchi katika kata 13 jijini Mbeya kati ya 36 zitakazo nufaika kwa lengo la uzalishaji wa kiuchumi na kutunza mazingira.

Miche hiyo imetolewa na Taasisi ya Tulia Trust kupitia Mkurugenzi wake Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson ikiwa ni mikakati yake ya kuifanya Mbeya kuwa ya kijani.

Akikabidhi miche hiyo kwa wananchi, watendaji wa Serikali na viongozi wa chama Mratibu wa zoezi hilo na Ofisa Uhusiano na Mawasiliano wa Taasisi hiyo, Addy Kalinjila amesema hilo ni zoezi endelevu na miche hiyo inatolewa bure.