Thursday, February 22, 2024

RAIS WA IPU DKT. TULIA AFANYA MAZUNGUMZO NA MKUU WA MKOA WA MBEYA


Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) ambae pia Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson, amefika Jimboni kwake na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera.

Mazungumzo hayo yamefanyika  katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa huku pamoja na  mambo mengine wamejadili kuhusu namna bora ya kuboresha Maendeleo ya  Jiji la Mbeya katika sekta mbalimbali.

Wakati huo huo Dkt. Tulia anatarajia kufanya zoezi la kugawa bima za afya bure kwa kaya 600 za jijini hapa.

Lengo ni kuhakikisha jamii inakuwa na afya njema sambamba na kukabidhi nyumba katika Kata ya Mwakibete iliyojengwa kuptia Taasisi yake ya Tulia Trust.

No comments:

Post a Comment