Monday, February 12, 2024

POLISI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA UWELEDI NA KUMTANGULIZA MUNGU.

Maafisa wa Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya wametakiwa kufanya kazi kwa weledi na kumtanguliza Mungu ili kufikia malengo ya Jeshi na Taifa kwa ujumla.

Hayo yamesemwa na Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Polisi SACP Robert Mkisi amewaasa leo Februari 12, 2024 alipotembelea Mkoa wa Mbeya na kukutana na mwenyeji wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ACP Benjamin Kuzaga na Maafisa wengine na kufanya mazungumzo.

Mkisi alipata kushika nyadhifa mbalimbali ndani ya Jeshi la Polisi ikiwemo Mkuu wa Shule ya Polisi Tanzania zamani CCP, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kigoma.

 

Kamishna Mkisi ameendelea kuwajengea uwezo wa utendaji kazi Maafisa, Wakaguzi na Askari Polisi katika nyanja mbalimbali ili kuleta uweledi na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Kipolisi.

No comments:

Post a Comment