Monday, February 12, 2024

AFISA MTENDAJI WA KATA AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUOMBA RUSHWA YA LAKI MBILI.

Afisa Mtendaji Kata ya Lusungo, Edestus Clemence Ndunguru amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kyela kwa shtaka la kuomba na kupokea Rushwa ya Tsh. 200,000 ili amsaidie Mwananchi kuongea na Askari Polisi waweze kumpa dhamana katika Kituo cha Ipinda.

Kosa hilo ni kinyume na kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa na 11 ya Mwaka 2007. Mshtakiwa alipelekwa Mahabusu kwa kutokutimiza masharti ya Dhamana huku Kesi ikiahirishwa hadi Februari 20, 2024.

No comments:

Post a Comment