Vyama vya Ushirika vya Wakulima wa tumbaku Wilaya ya Chunya na Songwe wamekerwa na Muungano wa Vyama Vikuu vya Ushirika Tanzania (TCJE) kuchelewesha pembejeo za kilimo na kutaka usambazaji ufanywe na Chama Kikuu cha Wakulima wa Tumbaku (CHUTCU) ili kunusuru uzalishaji.
Kauli hiyo imetolewa jana February 29, 2024 kwenye Mkutano mkuu wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Tumbaku (CHUTCU) ambapo wamedai TCJE kutowafikishia mbolea kwa wakati wakuwa chanzo cha kusababisha mazao yao yasifanye vizuri shambani.
Meneja Mkuu wa Chama cha kikuu cha wakulima wa Tumbaku (Chutcu)Wilaya ya Chunya Christian Msingwa (kulia)akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mbaraka Batenga.
Mkulima na Mwanachama wa CHUTCU, mawazo mamboleo amesema changamoto ya TCJE kuchelewesha pembejeo zimekuwa zilizoathiri kwenye uzalishaji wa tumbaku na hawakubaliani na TCJE kuendelea kusambaza pembejeo za kilimo badala yake chama kikuu cha ushirika CHUTCU ndio kiwe kinasimamia.