Jaffary Haniu, Mkuu wa Wilaya ya Rungwe.
Mkuu
 wa Wilaya ya Rungwe Jaffary Haniu amekemea vitendo vya ukatili kwa 
watoto na jamii kwa ujumla ambavyo kwa namna moja au nyingine 
vinachangia kuongezeka kwa maambukizi ya UKIMWI.
Akihutubia 
katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ambayo kwa Mkoa ya Mbeya 
yamefanyika Wilayani Rungwe, Haniu ametaja vitendo ukatili kuwa ni 
pamoja na ubakaji ulawiti na ukeketaji katika baadhi ya  mikoa nchini 
Tanzania.
Mganga Mkuu mkoa wa Mbeya Dkt. Maisara Karume ametaja juhudi zinazofanywa na Mkoa katika kutokomeza ugonjwa huo 8ni pamoja na kufanya tohara kwa wanaume ambayo imethibika kuwa ina uwezo wa kuzuia maambukizi kwa asilimia 60%, pia kutoa elimu na matumizi ya kondomu na kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa kujifungua.


No comments:
Post a Comment