Friday, December 8, 2023

MAADHIMISHO YA MIAKA 62 YA UHURU WA TANGANYIKA.

Kuelekea maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanganyika, Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe inakusudia kuadhimisha siku hiyo kwa namna tofauti kwa kufanya usafi wa mazingira, upandaji miti na michezo mbalimbali.

Akiongea na waandishi wa habari Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Jaffary Haniu amewahamasisha wananchi kushiriki shughuli za usafi, upandaji miti na michezo mbalimbali sambamba na kudumisha amani na utulivu iliyoachwa na waasisi wa Taifa letu.

Maadhimisho hayo yatafanyika katika viwanja vya Tandale Tukuyu Mjini ambapo pamoja na mambo mengine itashuhudiwa michezo mbalimbali ikifanyika.

Kauli mbiu katika maadhimisho hayo kwa mwaka huu ni "Umoja na mshikamano ni chachu ya maendeleo ya Taifa letu".

No comments:

Post a Comment