Saturday, December 2, 2023

WANANCHI WATAKIWA KUACHA UTAMADUNI WA KUHIFADHI MAJUMBANI MIILI YA NDUGU ZAO WALIOFARIKI.

Wananchi Wilayani Mbarali wametakiwa kuacha utamaduni wa kuhifadhi majumbani miili ya wapendwa wao waliopoteza maisha na badala yake wawapeleke katika vituo vya kutokelea huduma za afya kwani serikali imeboresha huduma za afya ikiwemo vyumba vya kuifadhia maiti.

Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Dkt. Ray Salandi mbele ya kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya ilipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya chama hicho katika sekta ya elimu na afya ukiwemo mradi wa jengo la kuhifadhi maiti ‘mochwari’ katika Hospitali ya Wilaya ya Mbarali.

Dkt. Salandi amesema serikali imenunua mashine nyingi za kuhifidhia maiti akivitaja vituo vya afya vya Madibila, Utengule Usangu na Rujewa kuwa kila kimoja kina mashine yenye uwezo wa kuhifadhi maiti tatu huku Hospital ya Wilaya ikiwa na mashine ya kuhifadhi miili kumi na mbili kwa wakati mmoja hivyo kama wilaya ina nafasi za kuhifadhi Maiti 21.

No comments:

Post a Comment