Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani ambae pia ni Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson amelazimika kuingilia kati mgogoro wa Kanisa la The Children of Gospel for All International (TCH-GOLFN) na Halmashauri ya Jiji la Mbeya  unaohusisha uhalali wa umiliki wa eneo linalopaswa kujengwa kanisa na kuweka zuio kwa kipindi kirefu sasa.
Dkt. Tulia ambae pia ni Mbunge wa Mbeya mjini amefikia hatua hiyo baada 
ya kusikia uwepo wa mgogoro huo uliodumu kwa zaidi ya 20 ukihusisha 
Halmashauri ya Jiji na kusababisha waumini wa kanisa hilo kutaka kumuona
 Rais Samia Suluhu Hassan kuingilia kati.
Akizungumza na waumini 
wa na Mchungaji wa kanisa hilo, John Ikowelo katika eneo lenye mgogoro 
Dkt. Tulia ametaka uongozi wa Jiji la Mbeya kupelekea nyaraka mbalimbali
 zinazoonyesha uhalali wa nani mmiliki wa eneo hilo.
Awali 
Mchungaji Ikowelo alimuonyesha Dkt. Tulia nyaraka mbalimbali za eneo 
hilo zikiwepo ambazo zilimtaka mchungaji huo kulipia gharama za kibali, 
hususani majina ya wananchi walio eneo kwa ajili ya kanisa na vikao 
mbalimbali vilivyobariki kuwepo kwa ujenzi wa nyumba hiyo ya ibada.
“Mh
 Spika na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) kwanza unisamehe 
nilikuruka kutoa taarifa za mgogoro huu kwako, pia waumini na uongozi wa
 kanisa tumekasirika sana na Serikali sababu kubwa ni watendaji wenu wa 
ngazi za chini ni shida sana na kuwa chanzo cha mgogoro” amesema 
Mchungaji Ikowelo.
Amesema kwa kuzingatia nyaraka hizo anaomba 
busara ya Serikali kuingilia kati ili haki itendeke wapewe kibali 
sambamba na kueleza kuna ujanja unaotaka kufanywa dhidi ya haki ya 
kanisa.
Kufuatia kauli hiyo, Dkt. Tulia alilazimika kumbana Ofisa
 mipango miji, Esau Dickley aeleze sababu za kutokutoa kibali cha ujenzi
 wa kanisa hilo, huku kukiwa na nyaraka mbalimbali za kubariki mradi wa 
nyumba ya ibada na viongozi mbalimbali wa serikali waliopita wakiwepo wa
 ngazi za serikali za mitaa.
“Sasa Leo nilikuja kwa ajili ya 
kutembelea kujiridhisha na kutoa maelekezo lakini sitoweza kwa sababu 
kuna mkanganyiko, mchungaji anazo nyaraka zote zinazo onyesha eneo hilo 
liko kisheria, sasa niwatake Jiji rejeeni na vielelezo vyote ili niweze 
kufanya maamuzi na haki itendeke.” amesema.
Dkt. Tulia amesema 
mara baada ya taarifa za Jiji kuwa tayari utaitishwa mkutano wa hadhara 
wa wananchi na kumtaka mchungaji kuja na watu waliotoa eneo kwa ajili ya
 ujenzi wa kanisa sambamba na wenyeji wanaojua historia ya eneo hilo.
  
Naye
 Naibu Meya wa Jiji la Mbeya, Kefasi Mwasote amehaidi kutoa ushirikiano 
wa kuhakikisha mgogoro huo inafikia kikomo sambamba na kuzisaka nyaraka 
zote tangu mgogoro huu kuanze miaka 20 iliyopita.
Naye Ofisa 
Mipango miji Jiji la Mbeya, Dickley amesema mgogoro huo ameugundua tangu
 mwaka 2017 ambapo lilipimwa na kubainika kuwa ni la shule.
Amesema
 kuwa Mchungaji alienda kuomba kibali ambapo wameshindwa kutokana na 
kubaini eneo hilo ni eneo Oevu sambamba na Jiji kuja na mipango kabambe 
wa mwaka 2025/30.
“Ili eneo lilipimwa na kupendekezwa 
litaendelezwa mpango kabambe la eneo oevu tangu mwaka 2019” Jambo ambalo
 lilipeleke Spika Dkt. Tulia kuhoji mpango huo ulipitishwa na nani awali
 ambalo limekosa majibu ya kujitoshereza na kutengeza mashaka.




No comments:
Post a Comment