Friday, December 29, 2023

SPIKA WA BUNGE AINGILIA KATI SAKATA LA MGOGORO WA KANISA NA HALMASHAURI YA JIJI LA MBEYA.

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani ambae pia ni Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson amelazimika kuingilia kati mgogoro wa Kanisa la The Children of Gospel for All International (TCH-GOLFN) na Halmashauri ya Jiji la Mbeya  unaohusisha uhalali wa umiliki wa eneo linalopaswa kujengwa kanisa na kuweka zuio kwa kipindi kirefu sasa.

Dkt. Tulia ambae pia ni Mbunge wa Mbeya mjini amefikia hatua hiyo baada ya kusikia uwepo wa mgogoro huo uliodumu kwa zaidi ya 20 ukihusisha Halmashauri ya Jiji na kusababisha waumini wa kanisa hilo kutaka kumuona Rais Samia Suluhu Hassan kuingilia kati.

Akizungumza na waumini wa na Mchungaji wa kanisa hilo, John Ikowelo katika eneo lenye mgogoro Dkt. Tulia ametaka uongozi wa Jiji la Mbeya kupelekea nyaraka mbalimbali zinazoonyesha uhalali wa nani mmiliki wa eneo hilo.
Awali Mchungaji Ikowelo alimuonyesha Dkt. Tulia nyaraka mbalimbali za eneo hilo zikiwepo ambazo zilimtaka mchungaji huo kulipia gharama za kibali, hususani majina ya wananchi walio eneo kwa ajili ya kanisa na vikao mbalimbali vilivyobariki kuwepo kwa ujenzi wa nyumba hiyo ya ibada.

“Mh Spika na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) kwanza unisamehe nilikuruka kutoa taarifa za mgogoro huu kwako, pia waumini na uongozi wa kanisa tumekasirika sana na Serikali sababu kubwa ni watendaji wenu wa ngazi za chini ni shida sana na kuwa chanzo cha mgogoro” amesema Mchungaji Ikowelo.

Amesema kwa kuzingatia nyaraka hizo anaomba busara ya Serikali kuingilia kati ili haki itendeke wapewe kibali sambamba na kueleza kuna ujanja unaotaka kufanywa dhidi ya haki ya kanisa.

Kufuatia kauli hiyo, Dkt. Tulia alilazimika kumbana Ofisa mipango miji, Esau Dickley aeleze sababu za kutokutoa kibali cha ujenzi wa kanisa hilo, huku kukiwa na nyaraka mbalimbali za kubariki mradi wa nyumba ya ibada na viongozi mbalimbali wa serikali waliopita wakiwepo wa ngazi za serikali za mitaa.

“Sasa Leo nilikuja kwa ajili ya kutembelea kujiridhisha na kutoa maelekezo lakini sitoweza kwa sababu kuna mkanganyiko, mchungaji anazo nyaraka zote zinazo onyesha eneo hilo liko kisheria, sasa niwatake Jiji rejeeni na vielelezo vyote ili niweze kufanya maamuzi na haki itendeke.” amesema.

Dkt. Tulia amesema mara baada ya taarifa za Jiji kuwa tayari utaitishwa mkutano wa hadhara wa wananchi na kumtaka mchungaji kuja na watu waliotoa eneo kwa ajili ya ujenzi wa kanisa sambamba na wenyeji wanaojua historia ya eneo hilo.
 
Naye Naibu Meya wa Jiji la Mbeya, Kefasi Mwasote amehaidi kutoa ushirikiano wa kuhakikisha mgogoro huo inafikia kikomo sambamba na kuzisaka nyaraka zote tangu mgogoro huu kuanze miaka 20 iliyopita.

Naye Ofisa Mipango miji Jiji la Mbeya, Dickley amesema mgogoro huo ameugundua tangu mwaka 2017 ambapo lilipimwa na kubainika kuwa ni la shule.

Amesema kuwa Mchungaji alienda kuomba kibali ambapo wameshindwa kutokana na kubaini eneo hilo ni eneo Oevu sambamba na Jiji kuja na mipango kabambe wa mwaka 2025/30.

“Ili eneo lilipimwa na kupendekezwa litaendelezwa mpango kabambe la eneo oevu tangu mwaka 2019” Jambo ambalo lilipeleke Spika Dkt. Tulia kuhoji mpango huo ulipitishwa na nani awali ambalo limekosa majibu ya kujitoshereza na kutengeza mashaka.

No comments:

Post a Comment