Sunday, December 31, 2023

AJALI YATOKEA SIMIKE: WATU KADHAA WAHOFIWA KUPOTEZA MAISHA.

Watu kadhaa wanahofiwa kufariki dunia katika ajali iliyotokea mapema leo Desemba 31, 2023 katika mteremko wa Simike eneo la Mbembela kata ya Nzovwe Jijijini Mbeya.

Ajali hiyo imehusisha magari manne ikiwemo lori kubwa la mizigo, basi ndogo mbili za abiria (Toyota Hiace) ambazo zilikuwa na abiria zikifanya safari kati ya Mbalizi na Sokomatola pamoja na gari ndogo aina ya Toyota Sienta.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, ACP Benjamin Kuzaga amekiri kutokea kwa ajali hiyo ambapo amesema kwa uchunguzi wa awali wamebaini kuwa chanzo cha ajali ni Lori lenye namba za usajili T 428 DXD kufeli breki kisha kugonga gari nyingine tatu zikiwemo Toyota Hiace mbili zinazofanya safari kati ya Mbalizi na Sokomatola zilizokuwa na abiria ndani yake.

No comments:

Post a Comment