Saturday, December 9, 2023

SAA TISA BARABARA YA MBEYA - TUNDUMA YAFUNGWA, WANANCHI WALILIA NJIA NNE.

Shughuli za usafirishaji wa abiria na mizigo zimekwama kwa zaidi ya saa tisa katika eneo la Simike barabara kuu ya Mbeya - Tuduma baada ya gari la mizigo kuanguka na kuziba njia.

Ajali hiyo imesababisha kuziba njia na kufanya shughuli za usafiri na usafirishaji kwenda mikoa na nchi jirani kusimama tangu saa 3:30 - hadi saa 12:00 baada gari hilo kuvutwa.

Lugano Asumwisye mkazi wa Uyole ameiomba serikali kuharakisha ujenzi wa barabara ya njia nne kwani ufinyu wa barabara imekua kero na kukwamisha shughuli za kiuchumi na kupoteza mapato ya serikali.

"Ni muda sasa tunasikia ujenzi wa njia nne utaanza ila tunaona hatua zinazochukuliwa zinaenda taratibu sana, serikali iliangalie hili kwa umuhimu wake linakwamisha mambo mengi, tangu saa tatu nipo hapa ningekua nimeshafika Tunduma na kuendelea na shughuli zangu".

Serikali inakusudia kujenga barabara ya njia nne itakayosaidia kupunguza msongamano wa magari kutoka Nsalaga hadi Ifisi (Km 29) barabara itayogharimu Bilioni 138.7.

No comments:

Post a Comment