Baadhi ya wachimbaji wamepaza sauti zao wakionesha masikitiko yao zaidi wakiituhumu Ofisi ya Madini Mkoa wa Songwe wakidai mchakato wa utoaji leseni umegubikwa na rushwa.

Nelson Kanunga mkazi wa Kampilipili amesema kilio chao ni kunyang’anywa eneo lao kwa dhuluma na maafisa madini kwani wamekuwepo eneo hilo yango mwaka 2011 ambapo zaidi ya watu elfu tatu wameathiriwa na mgogoro huo na kuhatarisha amani hivyo amemuomba Waziri wa Madini na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuingilia kati.


























