Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira akitoa maelekezo kwa watendaji wa mmoja wa migodi alitotembelea Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya.
Serikali imepiga marufuku shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu na kuchenjua katika Mto Zira Kata ya Ifumbo Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya mpaka wataalam watakapofika kufanya tathimini ya mazingira.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Seleman Jaffo, amesema hayo juzi wilayani Chunya wakati akiwa kwenye ziara ya kutembelea Kampuni ya G&I ambayo ilisitishiwa uzalishaji katika mto huo.
Jaffo amesema katika ziara yake miongoni mwa maeneo yaliyo msukuma ni kujiridhisha shughuli za uchimbaji zinazofanywa kwenye mto huo, sambamba na kutoa mwelekeo wa Wizara kutoruhusu shughuli hizo mpaka wataalam watakapofanya tathimini.























