Sunday, January 21, 2024

WAZIRI JAFFO APIGA MARUFUKU UCHIMBAJI WA DHAHABU NDANI YA MTO ZIRA WILAYANI CHUNYA.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira akitoa maelekezo kwa watendaji wa mmoja wa migodi alitotembelea Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya.

Sehemu ya bwawa linalotumika kutililisha tope lenye maji yenye kemikali ikiwa ni utekelezaji wa takwa kisheria.

Serikali imepiga marufuku shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu na kuchenjua katika Mto Zira Kata ya Ifumbo Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya mpaka wataalam watakapofika kufanya tathimini ya mazingira.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais  Muungano na  Mazingira Seleman Jaffo, amesema hayo juzi wilayani Chunya wakati akiwa kwenye ziara ya kutembelea Kampuni ya G&I ambayo ilisitishiwa uzalishaji katika mto huo.

Jaffo amesema katika ziara yake miongoni mwa maeneo yaliyo msukuma ni kujiridhisha  shughuli za uchimbaji zinazofanywa kwenye mto huo, sambamba na kutoa mwelekeo wa Wizara kutoruhusu shughuli hizo mpaka wataalam watakapofanya tathimini.

MASACHE AKABIDHI GARI LA WAGONJWA HOSPTALI YA WILAYA CHUNYA.


Mbunge wa Jimbo la Lupa Masache Kasaka amekabidhi gari la Wagonjwa kwa uongozi wa Hosptali ya Wilaya ya Chunya ambayo ilipandishwa hadhi kutoka kituo cha afya.

Masache amesema gari hilo la wagonjwa (Ambulance) limetolewa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuboresha huduma za afya katika vituo vya Kambikatoto na Lupa Wilayani humo.

Amesema Serikali itaendelea kuboresha sekta ya afya ambapo imetoa zaidi ya Sh 2.5 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa majengo nane sambamba na Sh 400 milioni kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba.

“Kama inavyofahamika hosptali hii awali ilikuwa kituo cha afya, Serikali ikapandisha hadhi na kuwa Kituo cha Afya, miundombinu yake ilikuwa sio rafiki lakini kwa kipindi cha miaka miwili tunashuhudia miundombinu imeboreshwa  chini ya Serikali ya awamu ya sita” amesema Masache.

Masache pia amewataka wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali sambamba na kuwataka kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mdogo wa Serikali za mitaa unaotarajia kufanyika hivi karibuni.

“Sitarajii kuona kuna watu wengine watachukua fomu kuwania nafasi hiyo kwani hawa waliopo wanatosha wameonyesha uwezo mkubwa kushiriki katika usimamizi wa miradi ya Maendeleo iliyoelekezwa na Serikali” amesema Masache.

Saturday, January 13, 2024

MRADI WA TACTICS WA BILIONI 85 KUGUSA MASOKO YA SOWETO NA SOKOMATOLA, JIJINI MBEYA.

Halmashauri ya Jiji la Mbeya iko mbioni kusaini mkataba wa ujenzi wa Soko la Soweto na Sokomatola kupitia mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Miji Tanzania (TACTIC) kwa ufadhiri wa Benki ya Dunia.

Akizungumza na Mwandishi wa habari leo Jumamosi, Januari 13, 2024 Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya, Dourmohamed Issa amesema tayari wameanza zabuni ya tenda kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya masoko hayo.

“Soko la Sokomatola na Soweto yanakwenda kujegwa kisasa zaidi na kutengeza taswira nzuri kwa Jiji la Mbeya na kabla ya mradi kuanza kuna maeneo yametengwa kwa ajili ya kuwahamishia wafanyabishara wanaopisha mradi huo” amesema Issa.

Wednesday, January 10, 2024

WANAUME KUTOSHIRIKI KLINIKI KUNACHANGIA KUTOTENGWA BAJETI ZA LISHE KATIKA FAMILIA

Wadau wakiwemo wazazi wakiwa katika kituo maalumu cha Malezi Jumuishi kilichofunguliwa na Taasisi ya WeCare Foundation kwaajili ya kutoa elimu ya afua za malezi stahiki kwa watoto ikiwemo lishe bora katika Hospitali ya Agakhan tawi la Mbeya. (Picha na Joachim Nyambo)

 

Hatua ya wanaume kutohudhuria kliniki wakati wenza wao wakiwa wajawazito au wanapokuwa wamejifungua inatajwa kuwa chanzo cha familia nyingi kutotenga bajeti ya milo sahihi kwa wanawake wajawazito, wanaonyonyesha na pia watoto wanaotimiza umri wa miezi sita tangu kuzaliwa.

 

Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa Makala haya umebaini kuwa licha ya wadau mbalimbali zikiwemo Taasisi binafsi na za serikali kutilia mkazo suala la uhamasishaji wanaume kuhudhuria kliniki pamoja na wenza wao bado mwamko ni mdogo.

 

Wadau wakiwemo wauguzi waliozungumzia hali hiyo wanasema ni wanaume wachache ambao wanaona umuhimu wa kwenda na wenza wao kliniki wanapokuwa wajawazito au wanapowapeleka watoto wachanga.

Sunday, December 31, 2023

AJALI YATOKEA SIMIKE: WATU KADHAA WAHOFIWA KUPOTEZA MAISHA.

Watu kadhaa wanahofiwa kufariki dunia katika ajali iliyotokea mapema leo Desemba 31, 2023 katika mteremko wa Simike eneo la Mbembela kata ya Nzovwe Jijijini Mbeya.

Ajali hiyo imehusisha magari manne ikiwemo lori kubwa la mizigo, basi ndogo mbili za abiria (Toyota Hiace) ambazo zilikuwa na abiria zikifanya safari kati ya Mbalizi na Sokomatola pamoja na gari ndogo aina ya Toyota Sienta.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, ACP Benjamin Kuzaga amekiri kutokea kwa ajali hiyo ambapo amesema kwa uchunguzi wa awali wamebaini kuwa chanzo cha ajali ni Lori lenye namba za usajili T 428 DXD kufeli breki kisha kugonga gari nyingine tatu zikiwemo Toyota Hiace mbili zinazofanya safari kati ya Mbalizi na Sokomatola zilizokuwa na abiria ndani yake.

Friday, December 29, 2023

SPIKA WA BUNGE AINGILIA KATI SAKATA LA MGOGORO WA KANISA NA HALMASHAURI YA JIJI LA MBEYA.

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani ambae pia ni Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson amelazimika kuingilia kati mgogoro wa Kanisa la The Children of Gospel for All International (TCH-GOLFN) na Halmashauri ya Jiji la Mbeya  unaohusisha uhalali wa umiliki wa eneo linalopaswa kujengwa kanisa na kuweka zuio kwa kipindi kirefu sasa.

Dkt. Tulia ambae pia ni Mbunge wa Mbeya mjini amefikia hatua hiyo baada ya kusikia uwepo wa mgogoro huo uliodumu kwa zaidi ya 20 ukihusisha Halmashauri ya Jiji na kusababisha waumini wa kanisa hilo kutaka kumuona Rais Samia Suluhu Hassan kuingilia kati.

Akizungumza na waumini wa na Mchungaji wa kanisa hilo, John Ikowelo katika eneo lenye mgogoro Dkt. Tulia ametaka uongozi wa Jiji la Mbeya kupelekea nyaraka mbalimbali zinazoonyesha uhalali wa nani mmiliki wa eneo hilo.

Wednesday, December 27, 2023

POLISI MBEYA YAWAFUATA WATOTO KANISANI NA KUTOA ELIMU YA KUZUIA UHALIFU.

Wazazi, walezi na jamii yatakiwa kushiriki kikamilifu katika utoaji wa malezi bora na elimu ya makuzi kwa watoto ili kuwajengea uwezo wa kujitambua, kujithamini na kujiepusha na vitendo viovu ikiwemo ukatili wa kijinsia na unyanyasaji dhidi yao.

Rai hiyo imetolewa Desemba 27, 2023 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi wa Polisi Benjamin Kuzaga katika kongamano la watoto wa Jimbo Kuu Katoliki Mbeya linalofanyika katika Parokia ya Mwanjelwa Jijini Mbeya.

Kuzaga amewataka wazazi na walezi kutimiza wajibu wao katika kuhakikisha wanawalinda watoto dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji na endapo wataona viashiria vya uhalifu huo watoe taarifa kwa viongozi wa dini na Jeshi la Polisi kwa hatua zaidi za kisheria.

Tuesday, December 26, 2023

TULIA TRUST YAGUSA WALEMAVU, WAZEE MAHITAJI YA CHAKULA NA KUBORESHA MAKAZI.

Taasisi ya Tulia Trust imekabidhi mahitaji ya chakula kwa wahitaji Wilayani Rungwe  kwaajili ya Sikukuu ya Krismasi.

Msaada huo uliokabidhiwa kwa kaya 13 ni pamoja na mchele, maharage na mafuta ya kula vyenye jumla ya thamani ya Sh. milioni 3.
Ofisa habari na Mawasiliano wa taasisi hiyo Joshua Mwakanolo amesema walengwa walionufaika ni ambao walibainika kwenye siku saba za kukimbiza bendera ya Upendo, Uwajibikaji na Mshikamano.

MABASI MATANO YAZUILIWA KUENDELEA NA SAFARI MBEYA KUTOKANA NA HITILAFU MBALIMBALI.

Jeshi la Polisi mkoani Mbeya limeyazuia mabasi matano ya abiria katika Stendi Kuu ya Mabasi Jijini Mbeya kuendelea na safari baada ya kukutwa na changamoto mbalimbali.

Akizungumza mapema leo Desemba 26, 2023 Mwanasheria Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani nchini, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Deus Sokoni baada ya kuendesha zoezi la ukaguzi wa Mabasi, Upimaji wa kilevi kwa madereva na utoaji wa elimu katika Stendi hiyo amesema jumla ya mabasi ya abiria 58 yamekaguliwa ambapo kati ya hayo mabasi matano kutoka kampeni ya TURU BEST, ISAMILO EXPRESS, ARUSHA EXPRESS, MSIGWA na AHMED yalikutwa na hitilafu katika mifumo mbalimbali ikiwemo mfumo wa breki.

“Jeshi la Polisi nchini kwa kushirikiana na mamlaka nyingine kama vile mamlaka ya udhibiti wa usafiri ardhini (LATRA) limepewa mamlaka ya kuzuia chombo cha moto kuendelea na safari pindi linapofanya ukaguzi na kugundua changamoto ikiwemo ubovu na hitilafu katika mifumo ya chombo hicho” amesema Sokoni.

Sunday, December 24, 2023

DKT. TULIA AHAMASISHA WENYEVITI, MADIWANI KUELEZEA UTEKELEZAJI ILANI YA UCHAGUZI 2020.

Rais wa Mabunge Duniani ambae pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson amehamsisha Madiwani, Wenyeviti wa Serikali za mitaa kwenda kufanya mikutano ya wananchi kueleza utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 2025.

Dkt. Tulia ambaye amesema hayo jana wakati akihutubia kwenye Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzo (CCM) Wilaya wenye  nia kuwahimiza upendo, umoja na mshikamano kwa lengo na  kukiimarisha chama kuelekea kwenye chaguzi mbalimbali.

Wednesday, December 20, 2023

MTANILA AMCOS CHUNYA KULIMA HEKTA 1,428 ZA TUMBAKU MSIMU WA 2024/2025.

Wakulima wa zao la Tumbaku Kata ya Lupa Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya wanatarajia kulima hekta 1428 sawa na ekari 3,571 za zao hilo kwa msimu wa kilimo 2024/25.

Hatua hiyo itapelekea kuchuma kilo milioni 1.3 mpka milioni mbili za tumbaku ambazo zitauzwa kwenye masoko ya uhakika ya ndani na nje ya nchi.

Mwenyekiti wa Bodi wa Chama cha Ushirika cha Wakulima wa Tumbaku (Mtanila AMCOS) Isaya Hussein amesema kwenye Mkutano mkuu wa mwaka uliolenga kupitia taarifa za utekelezaji wa masuala mbalimbali ya maendeleo katika umoja huo.

Saturday, December 16, 2023

KAMPENI YA 'AFYA CHECK' YAVUTIA VIJANA KUPIMA VVU KWA HIARI MKOANI MBEYA.

Kundi kubwa la vijana Mkoa wa Mbeya limejitokeza kwenye kampeni ya Afya Check kwa ajili ya kupima afya na kujitambua kama wana maambukizi ya virusi vya UKIMWI (VVU).

Kampeni hiyo yenye lengo la kuhamasisha vijana kwenye vyuo vya elimu ya juu 9 na kufikia vijana 4,000 Jijini Mbeya kwa ufadhiri wa Shirika la HJMRI ambayo inaendeshwa kwa makundi mbalimbali mkoani hapa.
Hatua hiyo imefikiwa kufuatia kundi kubwa la vijana kuwa kwenye hatari ya kupata maambukizi ya VVU huku kati ya kundi la watu 10 mmoja hukutwa na maambukizi sambamba na Mkoa kushika nafasi 2 kitaifa kwa kuwa na asilimia 9.3.

Thursday, December 14, 2023

TULIA TRUST YAHITIMISHA ZOEZI LA KUPEPERUSHA BENDERA YA UPENDO.

Ofisa Habari na Mawasiliano wa Taasisi ya Tulia Trust Joshua Mwakanolo (kulia) akikabidhi mahitaji mbalimbali kwa ajili ya wodi ya mama na mtoto katika Hosptali ya Makandana Wilaya ya Rungwe Mkoa Mbeya jana Alhamisi Desemba 13, 2023.

Taasisi ya Tulia Trust jana imehitimisha zoezi la kupeperusha bendera yenye ujumbe maalum wa Upendo, Uwajibikaji kwa jamii Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya ambayo ilianza kupeperushwa Desemba 9 mwaka huu.

Ofisa Habari na Mawasiliano, Joshua Mwakanolo amesema leo wilayani humo wakati akikabidhi mahitaji mbalimbali kwa wodi ya mama na mtoto katika Hospitali ya  Wilaya ya Makandana.