Sunday, August 4, 2024

TaCRI YAJA NA MIKAKATI KUKABILIANA NA KONOKONO KWENYE KAHAWA


Taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) imesema imekuja na mikakati ya kudhibiti wadudu waharibifu wa zao hilo wakiwepo konokono.

Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa Kanda (TacRI) Dismas Pangalas kwenye viwanja vya John Mwakangale vya maonyesho sikukuu ya wakulima Nanenane ambayo  yanafanyika kikanda mkoani hapa.

Amesema wadudu aina ya konokono wamekuwa na athari kubwa na tathimini za awali zinaonyesha kuwepo kwa mashambulizi yanaweza kusababisha kupoteza miche ya kahawa huku asilimia mbili mpaka tatu uharibiwa.

Monday, July 29, 2024

WANANCHI ISYESYE WAMSHUKURU DKT. TULIA KUGUSA WAHITAJI

Wananchi kata ya Isyesye jijini Mbeya wamesema kitendo cha Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Dkt. Tulia Ackson kusaidia wahitaji akiwepo mtoto kwenye ulemavu Jane Ambilikile (13) ni kujishusha kwa wananchi wasiojiweza.

Kauli hiyo wameitoa jana kwa nyakati tofauti mara baada ya kukabidhi nyumba mbili za wahitaji kwa familia ya Familia ya Damiani Mbwiga (50) na baiskeli mbili kwa walemavu akiwepo Mtoto Janeth Ambilikile (13) vilivyotolewa kupitia Taasisi ya Tulia Trust.

Akizungumza kwa niaba ya Wananchi Tabu Joel amesema kwa nafasi yake ya juu licha ya ubunge amekuwa ni kiongozi wa kipeke anawafuta machozi wanyonge wasio jiweza tofauti jamii inayo wazunguka.


Friday, July 26, 2024

KITUO CHA MIONZI KUJENGWA JIJINI MBEYA

Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kwa kushirikiana na Taasisi ya Saratani (Ocean Road) wanatajia kujenga kituo cha mionzi na kusimika mashine za kisasa.

Mkurugenzi mtendaji wa Hosptali ya Rufaa Kanda Dkt. Godlove Mbwanji amesema mara baada ya kutembelea kitengo cha huduma za mifumo ya chakula hosptalini hapo na kuona huduma mbalimbali za kitabibu zinazotolewa.

Amesema kitendo cha Serikali kubariki ushirikiano wa Taasisi ya Saratani Ocen Road Hosptali ya Rufaa Kanda kusimika mashine za mionzi utasaidia kuwapunguzia gharama wagonjwa kusafiri umbali mrefu kufuata huduma.

Wednesday, July 24, 2024

TANZANIA KUNUFAIKA NA MAFUNZO NCHINI INDIA

Bunge la India limeahidi kutoa fursa zaidi za mafunzo ya kuwajengea uwezo Watumishi wa umma kupitia Taasisi yake ya Utafiti na Mafunzo ya Kidemokrasia (PRIDE) inayoendeshwa na Bunge hilo.

Ahadi hiyo imetolewa jana Julai 23, 2024 na Spika wa Bunge la India (Lok Sabha), Om Birla wakati wa mazungumzo yake na Spika wa Bunge la Tanzania ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Dkt. Tulia Ackson katika Ofisi za Bunge hilo Jijini New Delhi.

Katika mazungumzo hayo pamoja na mambo mengine, Birla amemuelezea Dkt. Tulia kuhusu maboresho yaliyofanywa na Taasisi hiyo ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya ufadhili kwa Watumishi wa umma kutoka nchini mbalimbali Duniani hususani wabunge na watumishi wa Mabunge ya nchi hizo.

 

MZRH KUBORESHA MIUNDOMBINU YA MAKUNDI MAALUM


Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya imesema itaendelea kuboresha miundombinu  rafiki ya huduma za  afya hususani upasuaji na macho kwa makundi maalum wakiwepo watu wenye  walemavu wa kusikia (viziwi).

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi mtendaji wa Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya (MZRH) Dkt. Godlove Mbwanji wakati akifunga mkutano ulioandaliwa na Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) Mkoa wa Mbeya.

Dkt. Mbwanji amesema katika kuhakikisha huduma bora za afya zinaboreshwa  kwa makundi maalum Hosptali ya Kanda imekuwa ya kwanza kuwa na mkalimani wa lugha ya alama ili waweze kupatiwa huduma rafiki za afya.

Tuesday, July 23, 2024

DCEA AONYA MADEREVA KUJIHUSISHA USAFIRISHAJI DAWA ZA KULEVYA

Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti  na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Aretas Lyimo ameonya madereva na makondakta  mabasi ya abiria  kujiepusha na tabia ya kusafirisha dawa za kulevya wakibainika hatua za kisheria zitachukuliwa na vyombo vya moto kutaifishwa.

Kamishna Jenerali, Aretas Lyimo amesema hayo mkoani Mbeya kwenye mkutano uluihusisha Kamati za Ulinzi na Usalama, wadau wa sekta ya afya na walaibu wa dawa za kulevya uliolenga uhamasishaji mapambano ya dawa za kulevya uliofadhiriwa na shirika la HJFMRI.

Amesema kwa sasa serikali imefanya mabadiliko ya sheria ya usafirishaji wa dawa za kulevya kwa kutaifisha vyombo vya moto na madereva na makondakta stahiki.

DKT. TULIA ADHURU KABURI LA BABA WA TAIFA WA INDIA

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 23 Julai, 2024 ametembelea na kuweka shada la maua kwenye makumbusho ya kaburi la Baba wa Taifa la India hayati Mahatma Gandhi yaliyopo Jijini New Delhi, India.

Monday, July 22, 2024

TAMASHA NGOMA ZA ASILI MSIMU WA NANE KUTIMUA KIVUMBI SEPTEMBA 2024

Taasisi ya Tulia Trust imeandaa Tamasha la ngoma za asili laa makabila mbalimbali ya asili  msimu wa nane litalofanyika septemba mwaka huu.

Tamasha hill litashirikisha washiriki kutoka Tanzania bara na viziwani lengo ni  kuenzi tamaduni na kuonyesha uhalisia wa makabila

Ofisa habari na mawasiliano wa Taasisi ya Tulia Trust, Joshua Mwakanolo amesema leo Jumatatu Julai 22, 2024 na kwamba tamasha hilo litafanyika kuanzia Septemba 26 mpaka 28 mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa zamani uliopo kata ya Iyela Jijini hapa.

TULIA TRUST YAMSAIDIA KIJANA ALIYESHINDWA KUJIUNGA NA KIDATAO CHA TANO KWA KUKOSA MAHITAJI

Taasisi ya Tulia Trust imetoa tabasamu kwa Mussa Mwashilindi (17) akiyekwama kujiunga kidato cha tano kwa kukosa mahitaji ikiwepo sare za shule, daftari na mengineyo.

Mussa ambaye anaishi dada yake na wadogo zake wawili baada ya mama yao mzazi kufariki ghafla na kuwaacha wakijitegemea wenyewe kuendesha maisha.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi mahitaji hayo, ofisa habari kutoka Idara ya habari taasisi ya Tulia Trust Addy Kalinjila amesema mwanafunzi huyo alichaguliwa kujiunga kidato cha tano shule ya sekondari ya Dkt. Tulia iliyopo Kata ya Itende Mbeya Mjini.

Thursday, July 18, 2024

HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA YAWEKA ALAMA MUHIMU KILELE CHA MLIMA KILIMANJARO

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya kanda Mbeya wameendelea kuipongeza Serikali staili ya kipekee kwa kuboresha huduma za afya nchi katika kuwa hudumia wananchi, pia kuiunga mkono Serikali kufanya utalii wa ndani kwa vitendo kama alivyofanya Rais Dkt. Samia kwenye Filamu ya The Royal Tour.

Akiongea juu  kilele cha Mlima Kilimanjaro kwa niaba Watumishi wa hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, Salum Msambaji ameleza kuwa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imetumia njia hiyo pia kuishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji wa zaidi ya Bilioni 26 katika kuboresha Miundombinu, vifaa tiba, na mashine katika Hospitali Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya pamoja na huduma za kibingwa na bingwa bobezi.

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya wameushukuru Uongozi wa Waziri Ummy Mwalimu (Mb) na wasaidizi wake wa Wizara ya Afya kwa ushirikiano na maelekezo mazuri wanaopatiwa ambapo yamesaidia utendaji kazi mzuri katika kuwahudumia wananchi wa Nyanda za Juu Kusini na nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika SADC zikiwemo Zambia na Malawi.

Vilevile, Salumu ameeleza kuwa nia nyingine ya watumishi wa hospitali ya rufaa ya kanda Mbeya kupandisa bendera hiyo ya MZRH ni pamoja na kuitangaza Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Kitaifa na Kimataifa kutokana na  Mlima Kilimanjaro kuwa ni mojawapo ya alama ya Taifa, kuwa ni mlima mrefu zaidi barani.

Monday, July 15, 2024

TANROADS MBIONI KUANZA UJENZI BARABARA YA MBALIZI - SHIGAMBA

Wakala wa barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Mbeya umesema unatarajia kuanza ujenzi wa barabara kwa kiwango cha rami kutoka Mbalizi hadi Shigamba na Umalila baada ya serikali kutoa bilioni 2.

Kaimu Meneja, TANROADS Mkoa wa Mbeya Mhandisi, Kamokene Sanke amesema leo Jumamosi Julai 13, 2024 wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Sanje kata ya Santilya wilayani Mbeya kwenye ziara ya Mbunge wa Mbeya vijijini Oran Manasse Njeza ya kusikiliza kero za wananchi.

Amesema Serikali Kuu chini Rais Samia Suluhu Hassan imetoa Sh 2 bilioni  kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hizo kwa kiwango cha rami kutoka Mbalizi mpaka Shigamba yenye urefu wa Km 52 ambayo inatarajia kuanza hivi karibuni.

Friday, July 12, 2024

MGANGA WA KIENYEJI MATATANI KWA KUZINI NA MAHARIM

Masumbuko Wenson Sompo (51) Mkazi wa Sangambi Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya amefikishwa Mahakama ya Wilaya kwa tuhuma za kuzini na maharim.

Akisoma hati ya mashitaka kesi ya jinai namba 19278/ 2024 Kaihwa Stephen Mayanja mbele ya Hakimu wa Wilaya ya Chunya James Mhanusi amesema mtuhumiwa alitenda kosa hilo juni 23, 2024 porini majira ya saa tisa usiku.

Mayanja amesema kosa hilo ni kinyume cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai kifungu cha 158 (1) (a) cha kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2022 ambapo mshitakiwa amekana kutenda kosa.

TULIA TRAST YAMPA TABASAMU MWANAFUNZI ELIMU YA SEKONDARI

Mwanafunzi wa kidato cha pili shule ya Sekondari Itagano Jijini Mbeya  Sikujua Dickson (16) amemuomba Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson kumsaidia ili atimize ndoto yake  kupata elimu kufuatia Mama yake mzazi kuficha sare za shule na kumfanyia vitendo vya ukatili.

Sikujua amesema leo Ijumaa Julai 12, 2024 Mara baada ya Taasisi ya Tulia Trust kumkabidhi mahitaji mbalimbali ikiwepo viatu, sare za shule sambamba na kumuondoa nyumbani kwa wazazi wake  kumuendeleza kielimu .

Sikujua amefikia kutoa ombi hilo baada ya kuchoshwa na tabia ya Mama yake mzazi kuficha sare za shule kwa lengo la kumkatisha masomo hali ambayo amesema apendezwi nayo.