Wednesday, June 18, 2025

NJEZA ATEMBELEA WAFIWA AJALI ILIYOUA 29 MLIMA IWAMBI

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini  Oran M. Njeza, amezitembele na kutoa mkono wa pole kwa familia za watu 29 waliofariki na majeruhi  wa ajali.

Ajali hiyo ilitokea  Juni 7, 2025 katika mtelemko mkali wa mlima Iwambi Wilaya ya Mbeya, baada ya ya lori lilokuwa limebeba shehena za unga kugonga  magari mawili yakiwepo ya abiria.

Katika ajali hiyo watu 28 walipoteza maisha papo hapo na wengine tisa kujeruhiwa na kukimbizwa katika Hosptali Teule ya Ifisi Wilaya ya Mbeya.


Wednesday, June 11, 2025

DC MALISA AMKABIDHI MEYA JIJI LA MBEYA KITABU MPANGO MKAKATI MIAKA MITANO

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Malisa amezindua mpango mkakati wa Dira ya miaka mitano ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya na kumkabidhi rasmi Meya Jiji la Mbeya Dour Mohamed  Issa

Makabidhiano hayo yamefanyika leo Jumatano Juni 11, 2025 katika ukumbi wa mikutano wa  mkapa jijini hapa, ikiwa ni uzinduzi wa mpango mkakati wa dira ya miaka mitano ya 2025/26 mpaka 2029/2039 kwa halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Dira hiyo imebeba vipaumbele 29 ikiwepo masuala ya elimu, afya  maboresho ya teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) ujenzi wa bandari ya nchi kavu, sekta ya afya na elimu na mengineyo mengi.


Malisa amepongeza wadau walio fanikisha Halmashauri ya Jiji kutekeleza  mkakati, huku akitaka kuweka kipaumbele katika uboreshwaji miundombunu ya masoko ili wafanya biashara waweze kufanya kazi masaa 24.

Monday, May 5, 2025

DC MALISA: WANANCHI CHANGAMKIENI FURSA UJIO MADAKTARI BINGWA BOBEZI 36 MBEYA

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Beno Malisa, amehamasisha wananchi kutumia fursa ya ujio wa Madaktari Bingwa  Bobezi wa Dkt Samia  kufanyiwa vipimo vya uchunguzi wa magonjwa.

Kambi ya madaktari bingwa bobezi imeanza leo Mei 5 mpaka  Mei 9, 2025 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya (Mbeya RRH) kwa  muda wa siku tano.

Amesema huduma hizo zitawanufaisha wananchi kutoka mikoa Nyanda za Juu Kusini  ikiwepo  Mbeya, Ruvuma Songwe, Songea  Njombe.

Awali mkazi wa Njombe Vaileth Kwese,amesema kitendo cha serikali kuwafikishia huduma kimewapunguzia gharama za kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu.

Friday, May 2, 2025

JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA LAKANUSHA KUMKAMATA MDUDE

MADAKTARI BINGWA BOBEZI WA SAMIA KUWEKA KAMBI HOSPTALI YA RUFAA MKOA MBEYA

Madaktari bingwa bobezi wa Mama Samia wanatarajia kuweka kambi ya siku tano ya kufanya uchunguzi wa magonjwa mbalimbali katika Hosptali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.

Kambi hiyo imeratibiwa na Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Hosptali ya Rufaa kanda ya nyanda za juu kusini katika mikoa ya Songwe, Njombe, Songwe na Mbeya .

Akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa Mei 2, 2025, Mganga mfawidhi wa Hosptali ya Rufaa Mkoa wa Mbeya Dkt. Abdallah Mmbaga amesema kambi hiyo itaanza Mei 5 mpaka 9 mwaka huu.

Amesema  madaktari bingwa bobezi wa Mama Samia wametoka katika Hosptali ya Taifa Muhimbili (MOI), Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Taasisi ya  Benjamin Mkapa na Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.


Dkt. Mmbaga amesema lengo ni kutoa huduma za kibingwa na kikobezi kwa wananchi wa mikoa ya nyanda za Juu Kusini hususani kwa wale wenye changamoto za kiafya zinazohitaji huduma za kitaalam.

Wednesday, April 30, 2025

DC MBARALI AMALIZA MGOGORO WA WAKULIMA, WAFUGAJI NA MWEKEZAJI SHAMBA LA NARCO MWATENGA


Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya Kanali Maulid Sulumbu amesikiliza kero Kitongoji cha Manzega Kijiji cha Kilambo Kata ya Mwatenga kuhusiana na mgogoro wa wananchi na mwekezaji David Kaaya wa Kampuni ya O.C Industrial Holdings katika shamba la NARCO.

Akifungua mkutano Mwenyekiti wa Kijiji cha Kilambo Mwakani Chagu mbali ya kushukuru ujio wa Mkuu wa Wilaya huku akiwataka wananchi kuwa watulivu.

Diwani wa Kata ya Mwatenga Omary Sagutangu amesema mgogoro wa mwekezaji na wananchi umedumu kwa muda mrefu hivyo ujio wa Mkuu wa Wilaya utakuwa suluhisho kwani vikao vingi vimefanyika katika ngazi mbalimbali bila mafanikio.

Frank Sichalwe Katibu Tawala Wilaya ya Mbarali amesema ofisi yake ilipokea malalamiko kutoka kwa wananchi hivyo kutokana na uzito huo Mkuu wa Wilaya amefika kwa ajili ya kuwasililiza.

Saturday, April 26, 2025

JOWUTA, THRDC WALAANI WANAHABARI KUKAMATWA NA KUPIGWA


Chama cha Wafanyakazi katika Vyombo vya Habari Tanzania (JOWUTA) na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binaadamu nchini (THRDC) wamelaani kuanza kuibuka matukio ya waandishi wa habari na watangazaji kukamatwa na baadhi kupigwa na hata kuharibiwa vifaa vyao vya kazi na vyombo vya dola.

Kauli ya kulaani imetolewa leo Aprili 25 mwaka huu na Mwenyekiti wa JOWUTA Mussa Juma leo mkoani Mbeya, wakati wa mafunzo kwa wanahabari kuhusu uandishi wa habari za uchaguzi, ulinzi na usalama kazini.

Mafunzo hayo yamehusisha waandishi kutoka mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe, ambapo Juma amesema matukio ya kukamatwa, kupigwa na kuharibiwa vitendea kazi hayakubaliki katika nchi inayojinadi kuwa inazingatia misingi ya kidemokrasia.

Sunday, April 20, 2025

“KWENYE UCHAGUZI HUU TUWE WATU WA KUSAMEHEANA” ASKOFU PANGANI ‎

Katika kuadhimisha Sikukuu ya Pasaka, Askofu wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi Robert Pangani amewataka waumini, viongozi wa serikali na dini kuwa na moyo wa msamaha kama ambavyo Mungu alivyousamehe ulimwengu kupitia Yesu Kristo aliyekufa na kufufuka kwa ajili ya mwanadamu.

‎Wito huo ameutoa katika maadhimisho ya ibada ya Sikukuu ya Pasaka iliyofanyika katika kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi Ushirika wa Ibala ulipo Halmashauri ya Jiji la Mbeya. 

Askofu Pangani amesema ili kuwa Mkristo   unayemwamini Mungu unapaswa kuwa na roho ya msamaha kwa kila mtu pasipo kujali kosa ulilofanyiwa.
‎Katika hatua nyingine amewataka watanzania kuendelea kuitunza amani ya nchi huku akiwataka wanasiasa kutokuwa na lugha za kuleta migogoro kwenye jamii kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu October, 2025 huku akisema utunzwaji wa amani unaanzia kwenye familia.
‎Kwa upande wake mchungaji wa ushirika wa Ibala Kanisa la Moravian Alinuwila Swillah amesema kila mtanzania anawajibu wa kulinda amani huku waumini walioshiriki ibada hiyo ya Pasaka wakisema viongozi wa dini wanapaswa kuwa mstari wa mbele kukemea uovu unatendeka kwenye jamii.

Wednesday, April 9, 2025

"TUPO TAYARI KWA UCHAGUZI, ILA TUNATAKA MABADILIKO HAYA" CHAUMMA

Pamoja na kuthibitisha kushiriki Uchaguzi Mkuu mwaka huu, Chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kimependekeza na kuishauri Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi baadhi ya mambo kufanyiwa marekebisho kabla ya zoezi hilo.

Tanzania inatarajia kufanya Uchaguzi Mkuu, Oktoba 25 mwaka huu kuwapata madiwani, wabunge na Rais, huku Chama hicho kikitarajia kusimamisha wagombea katika nafasi zote.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa Aprili 7, 2025, Katibu Mwenezi wa Chama hicho Taifa, Ipyana Njiku amesema katika kikao cha Halmashauri kuu ya Chama hicho Februari 19, 2025 kiliazimia kushiriki uchaguzi huo katika nafasi zote na kutoa mwelekeo wa nchi kwa miaka mitano ijayo.

Thursday, March 20, 2025

SUGU: NO REFORM NO ELECTION SIO KUSUSIA UCHAGUZI

ENG. MAHUNDI AANZA ZIARA KUKAGUA HUDUMA ZA MAWASILIANO MPAKA WA KASUMULU NA TUNDUMA

Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) amewasili katika ofisi za Mkoa wa Mbeya na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa huo, Dkt. Juma Homera, leo Machi 20, 2025.

Akimkaribisha Naibu Waziri Mahundi, Mkuu wa Mkoa, Dkt. Homera, ameipongeza wizara kwa kazi nzuri inayofanya katika kuboresha hali ya mawasiliano mkoani humo.

Dkt. Homera ameomba Wizara kuhakikisha maeneo ya Utalii yanakuwa na mawasiliano bora zaidi ili kuchochea Sekta ya Utalii, pamoja na kuendelea kuboresha huduma za mawasiliano katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo, ikiwemo Kyela.

Kwa upande wake, Mhandisi Mahundi amesema ziara yake inalenga kukagua upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo ya mpakani ya Kasumulu uliopo Mkoa wa Mbeya na Tunduma, mkoani Songwe, ambapo wakazi wa maeneo hayo wamekuwa wakikumbana na changamoto ya kupokea taarifa kutoka mitandao ya nchi jirani badala ya Tanzania.

Friday, February 21, 2025

HASHIM RUNGWE KUFANYA MKUTANO WA HADHARA MBEYA, UBWABWA BURE

 
Chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kinatarajia kufanya Mkutano wa hadhara Februari 22, 2025 Mwanjelwa Jijini Mbeya mkutano utakaoongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho Hashim Rungwe.

WATU WATANO WAKAMATWA KWA KUJIHUSISHA NA BIASHARA YA UPATU MTANDAONI

 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya linawashikilia watu wa tano wa kampuni ya LBL kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya upatu mtandaoni bila kuwa na kibali na kuwashawishi wateja kulipa fedha.

KENGOLD vs KMC, TIMU ZAELEZA JINSI ZILIVYOJIPANGA KUONDOKA NA ALAMA TATU

 

Kuelekea mechi ya KenGold dhidi ya KMC itakayochezwa kesho Februari 22, 2025 saa nane mchana katika uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya makocha wa timu zote wameeleza namna walivyojiandaa kuondoka na alama tatu muhimu katika mchezo huo.

Tuesday, February 18, 2025

WANANCHI WATAKIWA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 2025


Wananchi wa jimbo la Mbeya vijijini wametakiwa kujipanga kikamilifu kushiriki katika uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 2025 ili kuchagua viongozi wataotekeleza miradi ya maendeleo.

Mbunge wa Jimbo la Mbeya vijijini Oran Njeza ametoa kauli hiyo jana Februari 18, 2025 wakati wa hafla ya kuwapongeza wenyeviti wa serikali za mitaa na vitongoji waliochaguliwa katika uchaguzi mdogo wa serikali za mitaa mwaka 2024.

Njeza, amepokelewa na maelfu ya wananchi wa Kata ya Isuto jimboni kwake amesema anawashukuru wananchi kwa kuwaamini viongozi hao kwa wakati mwingine ili kuunga mkono juhudi za serikali kuwaletea maendeleo.

 

Monday, February 17, 2025

CHIEF GODLOVE ADHAMINI MASHINDANO YA UMITASHUMTA KYELA

Timu 120 kutoka Shule mbalimbali za msingi wilayani Kyela Mkoa wa Mbeya zimeshiriki Mashindano ya Michezo ya Taaluma Tanzania (UMITASHUMTA) yaliyoanza kutimua kivumbi jana kwenye viwanja tofauti.

Mdhamini mkuu wa mashindano hayo, mdau wa michezo nchini, Chief Godlove Mwakibete ambaye mbali na udhamini amechangia mahitaji mbalimbali na zawadi kwa washindi.

Akizungumza na waandishi wa habari, amesema ameguswa kudhamini lengo ni kuunga mkono juhudi za serikali kuhamasisha michezo na kuibua vipaji vya vijana mashuleni na kuviendeleza.

"Vijana tunahitaji kuunga mkono serikali kuwekeza katika michezo kwa kuibua vipaji vya wanafunzi na kuvikuza kupitia michuano mbalimbali kwa kutambua michezo nia afya, michezo ni fursa ya ajira" amesema Mwakibete.

Thursday, February 13, 2025

NJEZA: BUNGE LIMESHAURI UKUSANYAJI KODI ZA MAJENGO UREJESHWE SERIKALI ZA MITAA

Mbunge wa Jimbo la Mbeya vijiji Oran Njeza ameishauri serikali kuondoa makusanyo ya kodi za majengo kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwenda serikali za mitaa.

Njeza amesema Bunge limeshauri kuhakikisha kiwango cha asilimia 20 ya mapato ya kodi za majengo zielekezwe kwenye Halmashauri kwa wakati.

Mbunge huyo ametoa kauli hiyo wakati akiwasilisha bungeni taarifa ya kamati ya bunge kwa mwaka wa fedha 2024.

Amesema katika mwaka fedha 2024/2025 serikali iongeze kiwango kinacho rejeshwa katika halmashauri kutoka asilimia 20 mpaka 50 ili kuharakisha zoezi la uthamishaji wa majengo na kurejesha asilimia 20.

Sambamba na hilo Mbunge Njeza amesema bunge limeshauri kuboreshwe mfumo wa tausi katika ukusanyaji wa mapato ya majengo sambamba na kuongeza idadi ya wataalamu ili kurahisisha utekelezaji.

Taarifa hiyo imeungwa mkono na wananchi huku wakieleza itawezesha kulipa kwa hiyari kodi ya majengo tofauti na makusanyo kupitia Mamlaka ya Mapato (TRA).

Tuesday, February 4, 2025

DC MALISA AHIMIZA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA KUPIMA SARATANI

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Beno Malisa amewataka wananchi kuwa na utamaduni wa kupima afya ili kukabiliana na ugonjwa saratani, huku takwimu zikionyesha watu 500 wamepatiwa huduma baada ya kubainika.

Malisa amesema hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera kwenye Maadhimisho ya siku Saratani Duniani yaliyofanyika leo Jumanne Februari 4, 2024 katika Hosptali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH).

"Niwasisitize wananchi kupima afya mara kwa mara tunaona takwimu zinaonyesha watu 500 wamegundulika kuwa na saratani hususani kwa wanawake na wanaume" amesema Malisa.