Monday, May 5, 2025

DC MALISA: WANANCHI CHANGAMKIENI FURSA UJIO MADAKTARI BINGWA BOBEZI 36 MBEYA

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Beno Malisa, amehamasisha wananchi kutumia fursa ya ujio wa Madaktari Bingwa  Bobezi wa Dkt Samia  kufanyiwa vipimo vya uchunguzi wa magonjwa.

Kambi ya madaktari bingwa bobezi imeanza leo Mei 5 mpaka  Mei 9, 2025 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya (Mbeya RRH) kwa  muda wa siku tano.

Amesema huduma hizo zitawanufaisha wananchi kutoka mikoa Nyanda za Juu Kusini  ikiwepo  Mbeya, Ruvuma Songwe, Songea  Njombe.

Awali mkazi wa Njombe Vaileth Kwese,amesema kitendo cha serikali kuwafikishia huduma kimewapunguzia gharama za kusafiri umbali mrefu kufuata matibabu.

Akizungumza na maelfu ya wananchi kwenye uzinduzi wa kambi hiyo, Malisa amesema ni matokeo ya uwekezaji wa Serikali ya awamu ya sita ikiwepo ununua vifaa na kuendeleza wataalamu wa kada za  afya.

"Niwashukuru wote mliojitokeza kupata huduma hizi, lakini mkawe mabalozi wazuri kwa wananchi wengi kueleza ujio madaktari bingwa bobezi wa magonjwa mbalimbali.

Malisa amewataka wakisubiri siku ya mwisho ambapo kutakuwa na wageni kutoka mikoa mbalimbali.

Mwenyekiti wa bodi ya ushauri Hosptali ya Mkoa  Dkt. Julius Kaijage, amesema wana kila sababu ya kuishukuru serikali kwa kusogeza huduma ambazo walikuwa wakutumia gharama kubwa kuzifuata.

Mganga Mfawidhi, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya Dkt. Abdallah Mmbaga amesema kambi hiyo madaktari bingwa na bingwa bobezi itadumu kwa siku tano na kueleza mkakati wao wa  kuwapatia ushirikiano mkubwa kwa kipindi hicho.

Miongoni mwa huduma za kibingwa zitakazo tolewa kwa wananchi wa ni pamoja na Ubingwa katika Magonjwa ya Watoto, Wanawake na Uzazi, Magonjwa ya Ndani.

No comments:

Post a Comment