Friday, June 20, 2025

HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA YAPOKEA MSAADA WA VIFAA VYA MATIBABU YA MACHO KWA WATOTO

 

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH) imepatiwa msaada wa vifaa tiba, vifaa saidizi na mashine ya kisasa ya Ultra Sound kwaajili ya kutoela matibabu ya macho wa watoto wanaofikishwa hospitali kwaajili ya matibabu, venye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 100, kutoka kwa Shirika la Kilimanjaro Center for Community Ophthalmology (KCCO) kama sehemu ya juhudi za kuboresha huduma za matibabu ya macho kwa watoto wa nyanda za juu kusini mwa Tanzania.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo Martin Mutayoba, Mwakilishi wa Shirika la KCOO Nyanda za Juu Kusini, amesema kuwa shirika hilo limekuwa likifanya kazi kwa karibu na hospitali (MZRH) kwa huduma za matibabu ya macho pia kupitia huduma mkoba za matibabu ya macho kwa watoto kwa ufanisi zaidi.

Ameongeza kuwa msaada huo ni matokeo ya ushirikiano wanaopatiwa hivyo amewataka watumiaji wa vifaa hivyo kuvihifadhi vizuri ili viendelee kufanya kazi kwa ubora.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa Mbeya Dkt. Uwesu Mchepange, ametoa shukrani kwa wadau wa maendeleo, hususan Shirika la KCOO, kwa msaada wa vifaa vya uchunguzi na matibabu venye thamani ya zaidi ya milioni 100 walivyopatiwa.

Ameongeza kuwa msaada huo umekuja kwa wakati muafaka, kwani utaongeza kasi ya utoaji huduma na kupunguza muda wa magonjwa kufuata huduma. Vifaa hivyo ni pamoja na mashine za upasuaji wa macho kwa watoto, ultrasound ya kupima macho, na vifaa vya macho saidizi, vyote vililenga kuboresha huduma ya matibabu ya macho kwa watoto.

Kwa upande wake Dkt. Barnabasi Mshangila, Daktari Bingwa Bobezi wa macho kwa watoto, amemshukuru Uongozi wa hospitali kwa ushirikiano mkubwa na ameeleza kuwa msaada huu utasaidia kuboresha huduma za matibabu ya macho kwa watoto, na kwamba hakutakuwa na haja yarufaa kupeleka watoto kupatiwamatibabu ya kibingwa sehemu nyingine, kwani huduma zitapatikana kwa karibu zaidi.

Pia, ameahidi kuwa vifaa hivyo vitatunzwa kwa umakini ili viweze kudumu na kutoa huduma kwa muda mrefu, na kuimarisha ustawi wa afya ya macho kwa watoto watakaofika kwaajili ya huduma.

No comments:

Post a Comment