Thursday, July 17, 2025

TULIA TRUST YAREJESHA TABASAMU FAMILIA NYUMBA ILIYOTEKETEA MOTO


Taasisi ya Tulia Trust inayojihusisha na uwekezaji  kiuchumi wananchi imeanza ukarabati wa nyumba ya familia ya Mzee Ayoub Wakazi wa Kata ya Nsalaga Jijijini hapa.

Nyumba hiyo iliteketea kutokana na janga la moto lililotokea hivi karibuni hali iliyosababisha kukosa mahala pa kuishi.


Ukarabati huo unatekelezwa na Taasisi ya Tulia Trust  ambayo Mkurugenzi wake ni Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson na Rais wa Mabunge Duniani (IPU), kupitia mpango wa Tulia Trust mtaani kwetu.

Mpango huo umekuwa na tija ya kurejesha tabasamu kwa wananachi wa Jiji la Mbeya zikiwepo kaya zisizojiweza, yatima na wazee.

No comments:

Post a Comment