Mwandishi wa Habari, David Nyembe (kushoto), akikabidhiwa fomu ya kuomba ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Isanga kuchaguliwa kuwa mgombea udiwani wa Kata hiyo katika Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba mwaka huu.
Nyembe amekabidhiwa fomu na Katibu wa CCM Kata hiyo Golden Ndolela leo Juni 29, 2025.
Hadi kufikia leo majira ya saa nne asubuhi jumla ya wagombea watatu tayari wamechukua fomu ya kuomba ridhaa ya chama hicho kuwania nafasi hiyo akiwemo aliyekuwa Meya wa Jiji la Mbeya Mh. Dormohamed Issa.
No comments:
Post a Comment