Monday, February 17, 2025

CHIEF GODLOVE ADHAMINI MASHINDANO YA UMITASHUMTA KYELA

Timu 120 kutoka Shule mbalimbali za msingi wilayani Kyela Mkoa wa Mbeya zimeshiriki Mashindano ya Michezo ya Taaluma Tanzania (UMITASHUMTA) yaliyoanza kutimua kivumbi jana kwenye viwanja tofauti.

Mdhamini mkuu wa mashindano hayo, mdau wa michezo nchini, Chief Godlove Mwakibete ambaye mbali na udhamini amechangia mahitaji mbalimbali na zawadi kwa washindi.

Akizungumza na waandishi wa habari, amesema ameguswa kudhamini lengo ni kuunga mkono juhudi za serikali kuhamasisha michezo na kuibua vipaji vya vijana mashuleni na kuviendeleza.

"Vijana tunahitaji kuunga mkono serikali kuwekeza katika michezo kwa kuibua vipaji vya wanafunzi na kuvikuza kupitia michuano mbalimbali kwa kutambua michezo nia afya, michezo ni fursa ya ajira" amesema Mwakibete.

Thursday, February 13, 2025

NJEZA: BUNGE LIMESHAURI UKUSANYAJI KODI ZA MAJENGO UREJESHWE SERIKALI ZA MITAA

Mbunge wa Jimbo la Mbeya vijiji Oran Njeza ameishauri serikali kuondoa makusanyo ya kodi za majengo kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwenda serikali za mitaa.

Njeza amesema Bunge limeshauri kuhakikisha kiwango cha asilimia 20 ya mapato ya kodi za majengo zielekezwe kwenye Halmashauri kwa wakati.

Mbunge huyo ametoa kauli hiyo wakati akiwasilisha bungeni taarifa ya kamati ya bunge kwa mwaka wa fedha 2024.

Amesema katika mwaka fedha 2024/2025 serikali iongeze kiwango kinacho rejeshwa katika halmashauri kutoka asilimia 20 mpaka 50 ili kuharakisha zoezi la uthamishaji wa majengo na kurejesha asilimia 20.

Sambamba na hilo Mbunge Njeza amesema bunge limeshauri kuboreshwe mfumo wa tausi katika ukusanyaji wa mapato ya majengo sambamba na kuongeza idadi ya wataalamu ili kurahisisha utekelezaji.

Taarifa hiyo imeungwa mkono na wananchi huku wakieleza itawezesha kulipa kwa hiyari kodi ya majengo tofauti na makusanyo kupitia Mamlaka ya Mapato (TRA).

Tuesday, February 4, 2025

DC MALISA AHIMIZA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA KUPIMA SARATANI

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Beno Malisa amewataka wananchi kuwa na utamaduni wa kupima afya ili kukabiliana na ugonjwa saratani, huku takwimu zikionyesha watu 500 wamepatiwa huduma baada ya kubainika.

Malisa amesema hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera kwenye Maadhimisho ya siku Saratani Duniani yaliyofanyika leo Jumanne Februari 4, 2024 katika Hosptali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH).

"Niwasisitize wananchi kupima afya mara kwa mara tunaona takwimu zinaonyesha watu 500 wamegundulika kuwa na saratani hususani kwa wanawake na wanaume" amesema Malisa.

Friday, December 27, 2024

MWEF YATOA MSAADA KWA HOSPITALI YA WAZAZI META

Taasisi ya Maryprisca Women Impowerment Foundation (MWEF) inayoongozwa na Naibu Waziri wa  Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mkurugenzi wa Taasisi Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi imetembelea Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kwa ajili ya kutoa msaada kwa wazazi waliojifungua siku ya sikukuu ya Christmas.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Maryprisca Women Impowerment Foundation Adam Simbaya amesema lengo la kutembea Hospitali ya wazazi Meta ni kumshukuru Mungu pia akianisha zawadi zilizotolewa kuwa ni pamoja na maziwa, sabuni, pampas na wipes.

Aidha Simbaya amesema wanaunga mkono juhudi zinazofanywa na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi ambaye amekuwa akiyagusa makundi mbalimbali yakiwemo ya wanawake na watoto.

Sunday, December 15, 2024

JAJI MWAMBEGELE "KUJIANDIKISHA KUWA MPIGA KURA ZAIDI YA MARA MOJA NI KOSA LA JINAI"

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi nchini imewaasa wananchi kujiepusha na kosa la kujiandisha zaidi ya mara moja kwenye daftari la kudumu la wapiga kura na kutakiwa kujiandikisha mara moja na kwenye kituo kimoja ili kuepuka uvunjaji wa sheria.

Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Jacob Mwambegele katika Mkutano wa Tume na Wadau wa Uchaguzi kuhusu uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura umefanyika Jijini Mbeya leo Disemba 15, 2024.

"Kujiandikisha kuwa mpiga kura zaidi ya mara moja ni kosa la jinai, 'mtu yeyote atakaeomba kuandikishwa zaidi ya mara moja atakuwa ametenda kosa la jinai na akitiwa hatiani adhabu yake ni faini isiyopungua kiasi cha shilingi laki moja na isiyozidi laki tatu au kutumikia kifungo kisichopungua miezi sita na kisichozidi miaka miwili gerezani au vyote kwa pamoja" amesema Jaji Mwambegele.

Thursday, December 12, 2024

DKT. TULIA APOKEA MASHINE YA UPASUAJI NA KITANDA KWA WAJAWAZITO

Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson, amekabidhiwa mashine ya upasuaji na kitanda cha kisasa kwa ajili ya wajawazito vyenye thamani ya Sh Milioni 102 .

Vifaa hivyo vimetolewa kwa kwa ajili ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya vilovyotolewa na wadau wa Maendeleo.

Dkt. Tulia amepokea vifaa hivyo kutoka kwa mwakilishi wa wadau hao Noelah Msuya jana Desemba 12, 2024 na kisha kukabidhi kwa uongozi wa Hosptali ya Rufaa ya Mkoa.

Dkt,Tulia ameipongeza Serikali kwa jitihada zake endelevu katika kuboresha sekta ya afya ikiwemo kujenga vituo vya  afya ili kuwasogezea wananchi wake huduma ya karibu.

WAKULIMA WATAKIWA KULIPA MADENI MSIMU 2023/24

Chama cha Msingi cha Ushirika cha Wakulima wa Tumbaku (Lualaje Amcos) kimewataka wakulima kulipa madeni kwa wakati ili kuepuka kupigwa mnada kwa mali zao ikiwepo mashamba .

Mwenyekiti wa Lualaje Amcos, Alberto Kacheza amesema leo Desemba 12, 2024 kwenye mkutano mkuu 41 wa mwaka wa kupitia taarifa mapato na matumizi hali ya uzalishaji kwa msimu huu wa kilimo.

Kacheza amesema kuna baadhi ya wakulima kwa makusudi wamekuwa wakilimbikiza madeni ya mikopo ya pembeo kwa makusudi hali inayopelekea kupata hati za mashaka

"Leo tumepitia taarifa mbalimbali sambamba na mwenendo Amcos yetu na kupendeleza masuala ya msimu wa kilimo 2024/25 katika uwekezaji wenye tija kwenye kilimo cha tumbaku na hatua za kuwachukulia wakulima wasiorejesha fedha za mikopo" amesema.

Friday, December 6, 2024

MHANDISI MARYPRISCA MAHUNDI ACHANGIA MIL. 3.4 NA TOFALI KIKUNDI CHA GWALUGANO ISANGE

Naibu Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi ameunga mkono juhudi za Kikundi cha UWT Gwalugano Isange chenye mtaji wa shilingi milioni tisini huku akikichangia shilingi milioni tatu na laki nne pia tofali elfu moja za saruji kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mradi.

Katika hotuba yake Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi amewataka wanawake kupendana na kuwataka waendelee kuwahamasisha wengine kujiunga ili kila mwanamke amiliki uchumi wake ambapo amewataka wanawake kuchangamkia mikopo inayotolewa na Halmashauri.

Mbali ya kukipongeza kikundi hicho amesema changamoto wazichukulie kama fursa akikazia kampeni yake ya wanawake na uchumi pia akiwahimiza kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan.

Friday, November 29, 2024

WENYEVITI WAONYWA KUTOKUWA CHANZO CHA MIGOGORO

Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya Mohamed Fakii ameonya wenyeviti wa serikali za mitaa kuepuka kuwa chanzo cha migogoro na badala yake kuimarisha ulinzi shirikishi na usalama wa raia na mali zao.
 
Mohamed amesema leo Novemba 28, 2024 wakati akiwa mgeni rasmi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Beno Malisa kwenye tukio la kuapishwa wenyeviti 181 na wajumbe 908 katika mitaa, vitongoji na kata.
 
Amesema wenyeviti baada ya kuapishwe wakawe chachu kwa wananchi na sio kugeuka wababe wakati wa kuwatumikia makujumu yako kwenye maeneo yao ya kazi.

Monday, November 25, 2024

BENKI YA PBZ YAUNGA MKONO UMOJA WA BAJAJI NA BODABODA

Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) imetoa pikipiki 10 zikiwepo za matairi matatu (bajaji) mbili kwa  umoja wa bajaji na bodaboda jiji la Mbeya kwa lengo la kuunga mkono juhudi za serikali kuwezesha vijana kujiajiri

Meneja Masoko na Uendelezaji wa Benki ya PBZ Mohamed Ismail amesema jana Novemba 25, 2024 mara baada ya kumkabidhi Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackon kwenye maadhimisho ya miaka 15 ya umoja wa bajaji Jiji la Mbeya yaliyo fanyika viwanja vya Mwenge.

Ismail amesema kwa kutambua vijana ni chachu ya maendeleo na namna gani Mbunge wetu na Spika Dkt. Tulia Ackson anavyowekeza kusaidia vijana kujiajiri.

DKT. TULIA, TFS WAZINDUA KAMPENI UPANDAJI MITI MILIONI MBILI

Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Dkt. Tulia Ackson amehamasisha jamii kugeukia matumizi ya nishati safi na kutunza mazingira kwa kupanda miti rafiki.

Dkt. Tulia ambaye ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) amesema jana Jumatatu Novemba 25, 2024 wakati uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji upandaji miti iliyohusisha Wakala wa Huduma za Misitu (TFS).

Amesema katika kampeni hiyo wanatarajia kupanda miti  milioni mbili ya kivuli yenye uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi

Kampeni hiyo imehusisha upandaji miti katika Taasisi za Serikali zikiwepo Shule za Msingi na Sekondari Mkoa wa Mbeya na kugusa kata 36.

JESHI LA POLISI MBEYA LATOA MAFUNZO KWA WAANDISHI WA HABARI

Kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024 nchini, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendesha mafunzo ya siku moja ya kuwajengea uwezo Waandishi wa Habari mkoani humo kuhusu masuala ya uchaguzi.

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo Novemba 23, 2024 katika ukumbi wa mikutano wa Benki kuu ya Tanzania Tawi la Mbeya, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga amesema kuwa Jeshi la Polisi lipo imara kuhakikisha linasimamia sheria, kanuni na taratibu wakati wa uchaguzi na halitasita kuchukua hatua kwa yeyote atakayebainika kukiuka.

Kamanda Kuzaga amewataka Waandishi wa Habari kuwa wazalendo na kutumia taaluma yao kuwajulisha wananchi mchakato mzima wa uchaguzi jinsi unavyoenda na kutoa elimu kuhusu haki na wajibu wa mpiga kura.

DKT. TULIA ACKSON ASHIRIKI IBADA MADHABAHU YA SAUTI YA UPONYAJI NA REHEMA ISYESYE JIJINI MBEYA

Rais wa Mabunge Duniani Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson ameshiriki ibada Kanisa la Baptist Isyesye Madhabahu ya Sauti ya Rehema na sauti ya uponyajiKata ya Isyesye huduma inayoongozwa na Mchungaji Patrick Mwalusamba ambapo amewahimiza Waumini kuendelea kuombea amani nchini huku akiwasisitiza kushiki uchaguzi utakaofanyika Novemba 27 mwaka huu.

Dkt. Tulia Ackson amesema Waumini wanawajibu wa kwenda kusikiliza kampeni za uchaguzi ili wapate viongozi watakaowaletea maendeleo katika mitaa yao. Pia ameipongeza huduma hiyo kwa namna inavyozidi kukua siku hadi siku.

Dkt. Tulia Ackson amesema Waumini wasiposhiriki kupiga kura wasiwe na sababu za kuwalaumu viongozi watakaochaguliwa kwa kuwa wao wameshindwa kuitumia fursa hiyo.