Katibu
 Tawala Mkoa wa Mbeya Mohamed  Fakii ameonya wenyeviti wa serikali za 
mitaa kuepuka kuwa chanzo cha migogoro na badala yake kuimarisha ulinzi 
shirikishi na usalama wa raia na mali zao.
Mohamed amesema leo Novemba  28, 2024 wakati akiwa mgeni rasmi kwa niaba 
ya Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Beno Malisa kwenye tukio la kuapishwa 
wenyeviti 181 na wajumbe 908 katika mitaa, vitongoji na kata.
Amesema wenyeviti baada ya kuapishwe wakawe chachu kwa wananchi na sio 
kugeuka wababe wakati wa  kuwatumikia makujumu yako kwenye maeneo yao ya
 kazi.
"Mbeya tuna ushindi wa asilimia 95 kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa 
 sasa baada ya kuapishwa rejeeni kutekeleza majukumu yenu kwa 
kumtanguliza Mwenyezi Mungu" amesema. 
 Kwa upande wake Mwenyekiti wake Mtaa wa Mwasyoge Limba Mwailubi 
amesema wanakwenda kutekeleza majukumu yao kwa vitendo na kujipanga 
katika uchaguzi Mkuu 2025.
"Tumeaminiwa na wananchi tumesikia maelekezo ya Katibu Tawala kwa  
kugusa makundi mbalimbali na kuibua  changamoto  katika ngazi ya 
jamii" amesema.
Mratibu wa Uchaguzi Jiji la Mbeya Gregory Emmanuel amesema Jiji  
limetulia na uchaguzi umekwenda vizuri kikubwa wanahimizwa
ushirikiano katika kuwafikia wananchi.
.jpg)
.jpg)
No comments:
Post a Comment