Kikao cha kupata maoni ya wadau mbalimbali juu ya kupata halmashauri mpya ya wilaya ambayo wamependekeza kuipa jina la halmashauri ya wilaya kitulo ni kutokana na changamoto ya upatikanaji wa huduma kutokana na umbali kutoka makao makuu ya halmashauri ya wilaya mama ya Makete.
Wananchi wameiomba selikali kuwepo na halmashauri mbili ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za kijamii ikiwemo vyeti ya kuzaliwa, vitambulisho vya NIDA, huduma benki na huduma nyingine za kijamii.
Mwenyekiti wa kikao hicho Bi. Rhoda Nsemwa ameiambia Mwananchi kuwa wananchi wasihofu kuhusu vigezo kwa kuwa serikali inaangalia mambo mengi hadi kufikia hatua ya kugawa eneo la kiutawala na kuwa halmashauri ya wilaya.



















