Thursday, May 30, 2024

SUGU AMGALAGAZA MSIGWA UENYEKITI CHADEMA KANDA YA NYASA


Mbunge wa zamani wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu), ameshinda nafasi ya kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa katika uchaguzi uliofanyika jana Mei 29, 2024 katika Mji mdogo wa Makambako.

Mbilinyi alishinda uchaguzi huo kwa kura 54 sawa na 51% akimshinda Mchungaji Peter Msigwa aliyekuwa akitetea nafasi hiyo aliepata kura 52 sawa na 49%. Nafasi ya Makamu Mwenyekiti alishinda Frank Mwakajoka, Mbunge wa zamani wa Tunduma.

No comments:

Post a Comment