Thursday, May 30, 2024

TIMU 32 KUWANIA MILIONI 11.4 ZA TULIA TRUST UYOLE CUP 2024

Mashindano ya mpira wa miguu maarufu kama Tulia Trust Uyole Cup 2024 yameanza kutimua vumbi jana Jumatano Mei 29, 2024  katika uwanja wa Mwawinji bonde la  uyole ya kati Jijini hapa.

Mashindano haya yanashirikisha timu 32 kutoka Jiji la Mbeya huku zawadi mbalimbali zikitolewa kwa washindi, sambamba na ugawaji wa vifaa vya michezo ikiwepo jezi, mipira kwa washiriki wa mashindano hayo.

Miongoni mwa zawadi zitakazotolewa kwa mshindi wa kwanza kitita cha Shilingi milioni tano, mshindi wa pili milioni, mshindi wa tatu atapata milioni mbili huku mshindi wa nne akiondoka na shilingi milioni moja.

Zawadi nyingine ni pamaoja na mfungaji bora Tsh 100,000/- kipa bora Tsh 100,000/- timu yenye nidhamu Tsh 100,000/- sambamba na kikundi bora cha ushangiliaji Tsh100,000/-.

Mashindano hayo yameandaliwa na Taasisi ya Tulia Trust ambayo Mkurugenzi wake ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya mjini Dkt. Tulia Ackson.

No comments:

Post a Comment