Wednesday, May 29, 2024

MBUNGE WA LUPA ARIDHISHWA UJENZI BARABARA YENYE UREFU KM 1.04

 

Mbunge wa Jimbo la Lupa Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya Masache Kasaka amefanya ziara ya  kukagua ujenzi wa miundombinu ya barabara yenye urefu wa kilometa 1.04.

Masache katika ziara yake ameambatana na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwepo katibu wa CCM Wilaya Msafiri Mayeye na kwamba barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha rami.


Amesema ameridhishwa na utelezaji wa mradi huo ambao umelenga kutekekeza ilani ya uchaguzi ya 2020/2025 yenye kuleta maendeleo kwa wananchi.

Amesema mpaka ukamilike utagharimu zaidi ya Sh 397 milioni  ambayo na Serikali na kukamilika kwa mradi huo utakuwa kiungo kikubwa cha kuchochea shughuli za kiuchumi na mapato ya Serikali.

No comments:

Post a Comment