Mbunge
 wa Jimbo la Lupa Masache Kasaka ameiomba Serikali kuboresha uwanja wa 
Sokoine uliopo Jijini Mbeya na pia kukamilishwa kwa ujenzi wa uwanja unapatikana katika kata ya Mbugani wilayani Chunya.
Masache ameyasema hayo Bunge Jijini Dodoma wakati akichangia hotuba ya makadirio ya bajeti ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo iliyowasilishwa na Waziri mwenye dhamana Dkt. Damas Ndumbaro.
 
"Mimi natoka 
Chunya, sisi tumepata bahati ya kupandisha timu ya ligi kuu msimu ujao 
KenGold FC, Mbeya sasa tuna timu mbili za ligi kuu Tanzania Prisons na KenGold 
FC, na timu moja ya daraja la kwanza Mbeya City, tunaiomba Serikali iboreshe 
uwanja wa Sokoine ili uwe bora zaidi, lakini pia sisi Chunya tulianza 
ujenzi wa uwanja wetu wa michezo, tunaiomba Serikali itupe fedha 
tukamilishe ule uwanja ili wanachunya waone sasa umuhimu wa kuwa na timu
 ya ligi kuu" amesema Masache. 
Mbali na hayo Masache ameongeza 
kuwa fursa mbalimbali zitaendelea kufunguka wilayani Chunya endapo 
uwanja ukikamilika kwa wakati na timu ya KenGold FC kuutumia katika michezo yao 
ya nyumbani.

No comments:
Post a Comment