Ikiwa
 ni siku ya kwanza ya kambi maalumu ya Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa 
Ubongo, Mgongo na Mishipa ya fahamu kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda 
Mbeya kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari Bingwa wa upasuaji wa 
mifumo ya fahamu, ubongo na uti wa Mgongo (Neurosurgeons) TNS, jana Aprili 08, 2024 wameanza rasmi zoezi la upasuaji kwa wagonjwa 3 
waliofika hospitalini hapo wakiwa na matatizo tofauti.
Katika 
moja ya wagonjwa waliofanyiwa upasuaji, madaktari Bingwa hao 
wamefanikiwa kumfanyia upasuaji mtoto wa siku 27 na kuondoa uvimbe wenye
 kilogramu 1.8 aliozaliwa nao sehemu ya nyuma ya kichwa chake upasujia 
uliochukua takribani saa moja kukamilika.
Mbali na upasuaji huo 
wataalam hao pia wamefanikiwa kuwafanyia upasuaji wagonjwa wawili mmoja 
akiwa ni mtoto mwenye umri miezi 9 aliyekuwa na tatizo la mgongo wazi na
 kufanikiwa kufunikwa eneo hilo kupitia upasuaji uliofanyika kwa muda wa
 saa moja, na mgonjwa mwingine ni mtu mzima mwenye umri wa miaka 39 
aliyevunjika pingili ya katikati ya uti wa mgongo baada ya kupata ajali 
na madaktari hao waliweza kufanikisha upasuaji huo uliochukua muda masaa
 mawili.
Kambi hiyo ya upasuaji wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya 
fahamu inaendelea kwa muda wa siku tano ndani ya Hospitali ya Rufaa ya 
Kanda Mbeya, ikilenga kutoa huduma hiyo kwa wananchi wa Nyanda za Juu 
Kusini ikiwemo mikoa ya jirani na Mbeya.



No comments:
Post a Comment