Sunday, January 28, 2024
MZRH YAWAKARIBISHA MADAKTARI BINGWA NA WAUGUZI WALIOKUA MASOMONI.
Saturday, January 27, 2024
MASHINDANO YA MBEYA TULIA MARATHON KUTIMUA VUMBI MEI 10 NA 11 SOKOINE, JIJINI MBEYA.
Tuesday, January 23, 2024
KT. TULIA AKABIDHI NYUMBA KWA MZEE MWENYE UHITAJI NONDE, JIJINI MBEYA.

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) ambaye pia ni Spika wa Bunge la Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini Dkt. Tulia Ackson amemkabidhi nyumba ya kuishi, kitanda na godoro Mzee Aswile Mwakigege mkazi wa Kata ya Nonde Jijini Mbeya.
Nyumba hiyo imekabidhiwa leo Jumanne Januari 23,2024 katika hafla fupi huku ikielezwa nyumba hiyo imejengwa kupitia taasisi yake ya Tulia Trust ambayo Dkt Tulia ni Mkurugenzi.
Hatua ya Taasisi hiyo kumjengea nyumba ,mara Mzee Aswile ni baada ya makazi aliyokuwa akiishi kubomoka na kupelekea mzee huyo kukosa makazi rasmi.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi nyumba hiyo, Dkt Tulia ameitaka jamii kuwakumbuka wazee wasiojiweza pale panapokuwa na mahitaji.
CHAKULA CHA MCHANA KWA WANAFUNZI KINAVYOLETA TIJA KATIKA UFUNDISHAJI
Halmashauri ya wilaya ya Rungwe kwa kushirikiana na wazazi imeendelea na Mpango wake kuhakikisha kila Mwanafunzi anapata chakula cha mchana kwa siku zote za masomo.
Monday, January 22, 2024
DKT. TULIA AKABIDHI MAHITAJI KWA WANAFUNZI 3,000 WANAOISHI KWENYE MAZINGIRA MAGUMU, JIJINI MBEYA.
“Kuna watu uwa wanajiuliza kwanini ninaposaidia watu lazima wapigwe picha,ni lazima kufanya hivyo lengo ni kuikumbusha jamii kusaidia wahitaji katika maeneo tunayotoka” amesema.
Sunday, January 21, 2024
WAZIRI JAFFO APIGA MARUFUKU UCHIMBAJI WA DHAHABU NDANI YA MTO ZIRA WILAYANI CHUNYA.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira akitoa maelekezo kwa watendaji wa mmoja wa migodi alitotembelea Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya.
Serikali imepiga marufuku shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu na kuchenjua katika Mto Zira Kata ya Ifumbo Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya mpaka wataalam watakapofika kufanya tathimini ya mazingira.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Seleman Jaffo, amesema hayo juzi wilayani Chunya wakati akiwa kwenye ziara ya kutembelea Kampuni ya G&I ambayo ilisitishiwa uzalishaji katika mto huo.
Jaffo amesema katika ziara yake miongoni mwa maeneo yaliyo msukuma ni kujiridhisha shughuli za uchimbaji zinazofanywa kwenye mto huo, sambamba na kutoa mwelekeo wa Wizara kutoruhusu shughuli hizo mpaka wataalam watakapofanya tathimini.
MASACHE AKABIDHI GARI LA WAGONJWA HOSPTALI YA WILAYA CHUNYA.
Masache amesema gari hilo la wagonjwa (Ambulance) limetolewa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuboresha huduma za afya katika vituo vya Kambikatoto na Lupa Wilayani humo.
Amesema Serikali itaendelea kuboresha sekta ya afya ambapo imetoa zaidi ya Sh 2.5 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa majengo nane sambamba na Sh 400 milioni kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba.
“Kama inavyofahamika hosptali hii awali ilikuwa kituo cha afya, Serikali ikapandisha hadhi na kuwa Kituo cha Afya, miundombinu yake ilikuwa sio rafiki lakini kwa kipindi cha miaka miwili tunashuhudia miundombinu imeboreshwa chini ya Serikali ya awamu ya sita” amesema Masache.
Saturday, January 13, 2024
MRADI WA TACTICS WA BILIONI 85 KUGUSA MASOKO YA SOWETO NA SOKOMATOLA, JIJINI MBEYA.
Akizungumza na Mwandishi wa habari leo Jumamosi, Januari 13, 2024 Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya, Dourmohamed Issa amesema tayari wameanza zabuni ya tenda kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya masoko hayo.
“Soko la Sokomatola na Soweto yanakwenda kujegwa kisasa zaidi na kutengeza taswira nzuri kwa Jiji la Mbeya na kabla ya mradi kuanza kuna maeneo yametengwa kwa ajili ya kuwahamishia wafanyabishara wanaopisha mradi huo” amesema Issa.
Wednesday, January 10, 2024
WANAUME KUTOSHIRIKI KLINIKI KUNACHANGIA KUTOTENGWA BAJETI ZA LISHE KATIKA FAMILIA
Wadau
wakiwemo wazazi wakiwa katika kituo maalumu cha Malezi Jumuishi
kilichofunguliwa na Taasisi ya WeCare Foundation kwaajili ya kutoa elimu
ya afua za malezi stahiki kwa watoto ikiwemo lishe bora katika
Hospitali ya Agakhan tawi la Mbeya. (Picha na Joachim Nyambo)
Hatua ya wanaume kutohudhuria kliniki wakati wenza wao wakiwa wajawazito au wanapokuwa wamejifungua inatajwa kuwa chanzo cha familia nyingi kutotenga bajeti ya milo sahihi kwa wanawake wajawazito, wanaonyonyesha na pia watoto wanaotimiza umri wa miezi sita tangu kuzaliwa.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa Makala haya umebaini kuwa licha ya wadau mbalimbali zikiwemo Taasisi binafsi na za serikali kutilia mkazo suala la uhamasishaji wanaume kuhudhuria kliniki pamoja na wenza wao bado mwamko ni mdogo.
Wadau wakiwemo wauguzi waliozungumzia hali hiyo wanasema ni wanaume wachache ambao wanaona umuhimu wa kwenda na wenza wao kliniki wanapokuwa wajawazito au wanapowapeleka watoto wachanga.