Wednesday, May 5, 2021

MV MBEYA II KUSITISHA SAFARI ZAKE KWA MUDA


Huduma za safari za meli ya Mv Mbeya II zimesitisha kwa muda kwaajili ya kuifanyia uchunguzi baada ya kupigwa na mawimbi hadi kupelekea kukwama kwenye mchanga ikiwa safarini katika Ziwa Nyasa.

Akizungumza na chombo kimoja habari leo Jumatano Mei 5, 2021 Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Claudia Kitta amesema abiria waliokuwa katika meli hiyo walioshindwa kurejea majumbani mwao baada ya tukio hilo watarejeshewa nauli zao, watapewa chakula na maradhi.

"Meli ya Mv Mbeya II kwa sasa haitoweza kuendelea na safari mpaka itakapofanyiwa uchunguzi wa kina wa kitaalam na tukijiridhisha itaruhusiwa kuendelea na safari na baadhi ya abiria wamewezeshwa sehemu ya maradhi ya chakula mpaka watakapoanza safari ya kwenda walikokuwa wakienda,” amesema Kitta.

Amesema kikao cha kamati ya ulinzi na usalama kitafanyika kwa ajili ya kufanya tathmini ya mahitaji ya Wananchi waliokuwa safarini mpaka uchunguzi wa meli hiyo utakapokamilika na kuendelea na safari.

Aidha, amesema baadhi ya abiria walipanda mabasi baada ya kurejeshewa nauli.

No comments:

Post a Comment