Saturday, May 22, 2021

WAHITIMU KIDATO CHA SITA 2021 WAITWA NA JKT


Wahitimu wa kidato cha sita mwaka 2021 wametakiwa kuhudhuria mafunzo kwa mujibu wa sheria katika kambi za Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) walizopangiwa  kuanzia Juni Mosi hadi 10, 2021.

Hayo yamesemwa jana Jumamosi Mei 22,  2021 na Kaimu mkuu wa utawala wa JKT, Kanali Hassan Mabena huku akizitaja kambi hizo kuwa ni Rwamkoma Mara, Msange Tabora, Ruvu Pwani, Mpwapwa, Makutupora Dodoma, Mafinga Iringa, Mlale, Itaka Songwe, Luwa, Milundikwa Rukwa, Nachingwea Lindi na Kibiti Pwani.

Kambi nyingine ni Oljoro JKT Arusha, Mgambo, Maramba Tanga, Makuyuni Arusha, Bulombora  na Mtabila Kigoma.

TULIA TRUST YASAIDIA UJENZI WA MATUNDU YA VYOO SHULE YA MSINGI ILOMBA

Na Ezekiel Kamanga.

Taasisi ya Tulia Trust inayoongozwa na Naibu Spika na Mbunge wa Mbeya Mjini Dkt Tulia Ackson imeungana na wananchi wa Kata ya Isyesye Jijini Mbeya katika ujenzi wa matundu nane ya vyoo shule ya msingi Ilomba inayokabiliwa na upungufu wa matundu ishirini na nane.

Zoezi hilo liliongozwa na Meneja wa Tulia Trust Jacqueline Boaz ambaye lengo ni kuunga mkono juhudi za wanachi wa Isyesye kwa kuchimba mtaro na kusomba mawe ili vyoo vikamilike kwa wakati ili kupunguza changamoto ya upungufu wa matundu ya vyoo katika shule hiyo.

"Hii si mara ya kwanza kutembelea shule hii mwaka 2019 Dkt Tulia alifika hapa kutoa msaada wa mifuko mia ya saruji na tanki la maji baada ya kupokea mahitaji kutoka kamati ya shule kwa ajili ya ukarabati wa madarasa", alisema Jacqueline.

Sunday, May 9, 2021

DKT. TULIA, MARYPRISCA, FYANDOMO WATOA MSAADA KWA WAHANGA WA MAFURIKO WILAYANI KYELA NA BUSOKELO

Pichani ni Naibu Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson (katikati), Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Maryprisca Mahundi (kulia), na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya Mh. Suma Fyandomo (kushoto).

 
HABARI NA EZEKIEL KAMANGA.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson, Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Maryprisca Mahundi ambaye ni Mbunge wa Wanawake Mkoa wa Mbeya na Suma Ikenda Fyandomo Mbunge wa Wanawake Mkoa wa Mbeya wamewatembelea kuwapa faraja na kutoa msaada wa chakula kwa wananchi waliokumbwa na mafuriko Wilaya ya Kyela na Busokelo Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.

Akitoa taarifa Kijiji cha Kisale Kata ya Ipinda kwa viongozi hao Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela Ezekiel Magehema alisema baadhi ya wananchi chakula kimeharibika, nyumba zao zimeboka pia mazao yamesombwa na maji hivyo wanawakati mgumu wa kujikimu ambapo baadhi wamehifadhiwa na ndugu zao.

Wednesday, May 5, 2021

MV MBEYA II KUSITISHA SAFARI ZAKE KWA MUDA


Huduma za safari za meli ya Mv Mbeya II zimesitisha kwa muda kwaajili ya kuifanyia uchunguzi baada ya kupigwa na mawimbi hadi kupelekea kukwama kwenye mchanga ikiwa safarini katika Ziwa Nyasa.

Akizungumza na chombo kimoja habari leo Jumatano Mei 5, 2021 Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Claudia Kitta amesema abiria waliokuwa katika meli hiyo walioshindwa kurejea majumbani mwao baada ya tukio hilo watarejeshewa nauli zao, watapewa chakula na maradhi.

"Meli ya Mv Mbeya II kwa sasa haitoweza kuendelea na safari mpaka itakapofanyiwa uchunguzi wa kina wa kitaalam na tukijiridhisha itaruhusiwa kuendelea na safari na baadhi ya abiria wamewezeshwa sehemu ya maradhi ya chakula mpaka watakapoanza safari ya kwenda walikokuwa wakienda,” amesema Kitta.

Amesema kikao cha kamati ya ulinzi na usalama kitafanyika kwa ajili ya kufanya tathmini ya mahitaji ya Wananchi waliokuwa safarini mpaka uchunguzi wa meli hiyo utakapokamilika na kuendelea na safari.

Aidha, amesema baadhi ya abiria walipanda mabasi baada ya kurejeshewa nauli.

Monday, May 3, 2021

UFAFANUZI WA SPIKA NDUGAI KUHUSU UBUNGE WA AKINA HALIMA MDEE NA WENZAKE

 

"Aandike barua aambatanishe na katiba ya chama chake, aniambatanishie na muhtasari wa hicho kikao kilichofanya hayo maamuzi, inawezekana huyo Katibu Mkuu kaamka tu kaandika halafu na mimi nakurupuka nachukua hatua, nitakua ni Spika au kitu cha ajabu, hivyo andika ili ile barua niwape watalam waangalie, halafu namuuliza msajili wa chama hawa wajumbe walioorodheshwa ndiyo wajumbe halisi?", amesema
 Spika Ndugai

UJUMBE WA BALOZI WA SWEDEN TANZANIA KWA UMOJA WA KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI TANZANIA

Balozi wa Sweden Tanzania, Mh. Anders Sjöberg.

"Mimi kama Balozi wa Sweden ninafurahi kuwepo leo kusherekea uhuru wa habari na kujieleza. Sweden na Tanzania ni marafiki wa siku nyingi, na wote tunatambua kwamba nguzo hii, sambamba na haki ya kupata taarifa ni muhimu sana kwa jamii inayoheshimu Demokrasia na Haki za Binadamu".

"Sweden inaamini kwamba maendeleo ya nchi yoyote ile yanapatikana kwa kupeana tarifa, kujadiliana kwa uwazi, na kuwajibishana. Basi sisi tutaendelea kuungana na watanzania wote katika jitihada za kukuza na kuendeleza uhuru wa habari na kujieleza nchini". Balozi Anders Sjöberg